Watumwa

Watumwa wote wawahesabu mabwana zao kuwa wanastahili hesh ima zote, ili watu wasije wakalitukana jina la Mungu pamoja na mafundisho yetu. Watumwa ambao mabwana zao ni waamini, wasikose kuwaheshimu kwa kuwa ni ndugu; bali watumike kwa ubora zaidi kwa sababu wale wanaonufaika kwa huduma yao ni waamini na ni wapendwa.

Fundisha na kuhimiza mambo haya. Mtu ye yote akifundisha kinyume cha haya na asikubaliane na maneno ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo, na mafundisho yanayo ambatana na kumcha Mungu, huyo amejaa majivuno na wala hafahamu cho chote. Mtu kama huyo ana uchu wa ubishi na mashindano ya maneno ambayo huleta wivu, ugomvi, matukano, shuku mbaya, na ugomvi wa mara kwa mara kati ya watu wenye mawazo maovu, ambao hawanayo ile kweli, na ambao hudhani kwamba kumcha Mungu ni njia ya kuchuma fedha.

Bali kumcha Mungu na kuridhika ni faida kubwa. Kwa maana hatukuja na kitu cho chote hapa duniani, wala hatuwezi kutoka na kitu. Lakini kama tuna chakula na mavazi, basi tutaridhika. Watu wanaotamani kuwa matajiri huanguka katika majaribu na mtego na katika tamaa nyingi mbaya na za kijinga, ambazo huwato komeza wanadamu katika upotevu na maangamizi. 10 Maana kupenda fedha ni chanzo cha uovu wote. Tamaa ya fedha imewafanya wengine watangetange mbali na imani na kuteseka kwa huzuni nyingi.

Mawaidha Ya Paulo Kwa Timotheo

11 Lakini wewe mtu wa Mungu, epuka haya yote. Tafuta kupata haki, utauwa, imani, upendo, subira na upole. 12 Pigana ile vita njema ya imani. Shikilia uzima wa milele ulioitiwa ulipokiri lile ungamo lako jema mbele ya mashahidi wengi.

13 Mbele ya Mungu ambaye amevipa vitu vyote uhai, na mbele ya Kristo Yesu ambaye kwa ushuhuda wake mbele ya Pontio Pilato alikiri lile ungamo jema, 14 ninakuamuru utunze amri hii bila doa wala lawama mpaka Bwana wetu Yesu Kristo atakapokuja. 15 Jambo hili Mungu atalitimiza kwa wakati wake mwenyewe, Mungu Mbarikiwa ambaye peke yake ndiye Atawalaye, Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. 16 Yeye peke yake ndiye asiyekufa, na ndiye aishiye katika nuru isiyoweza kukaribiwa; hakuna mwanadamu ali yepata kumwona wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye hata milele. Amina.

17 Uwaagize matajiri wa ulimwengu huu waache kujivuna, wala wasiweke matumaini yao katika mali ambayo haina hakika. Bali wam tumaini Mungu ambaye hutupatia vitu vyote kwa wingi ili tuvifu rahie. 18 Waambie watende wema, wawe matajiri katika matendo mema, wawe wakarimu na tayari kushiriki mali zao na wengine. 19 Kwa njia hii watajiwekea msingi imara kwa wakati ujao na hivyo watajipatia uzima ambao ni uzima kweli.

20 Timotheo, tunza vema yote uliyokabidhiwa. Epuka majadil iano yasiyo ya Mungu na mabishano ambayo kwa makosa huitwa elimu.

All who are under the yoke of slavery should consider their masters worthy of full respect,(A) so that God’s name and our teaching may not be slandered.(B) Those who have believing masters should not show them disrespect just because they are fellow believers.(C) Instead, they should serve them even better because their masters are dear to them as fellow believers and are devoted to the welfare[a] of their slaves.

False Teachers and the Love of Money

These are the things you are to teach and insist on.(D) If anyone teaches otherwise(E) and does not agree to the sound instruction(F) of our Lord Jesus Christ and to godly teaching, they are conceited(G) and understand nothing. They have an unhealthy interest in controversies and quarrels about words(H) that result in envy, strife, malicious talk, evil suspicions and constant friction between people of corrupt mind, who have been robbed of the truth(I) and who think that godliness is a means to financial gain.

But godliness with contentment(J) is great gain.(K) For we brought nothing into the world, and we can take nothing out of it.(L) But if we have food and clothing, we will be content with that.(M) Those who want to get rich(N) fall into temptation and a trap(O) and into many foolish and harmful desires that plunge people into ruin and destruction. 10 For the love of money(P) is a root of all kinds of evil. Some people, eager for money, have wandered from the faith(Q) and pierced themselves with many griefs.(R)

Final Charge to Timothy

11 But you, man of God,(S) flee from all this, and pursue righteousness, godliness,(T) faith, love,(U) endurance and gentleness. 12 Fight the good fight(V) of the faith. Take hold of(W) the eternal life(X) to which you were called when you made your good confession(Y) in the presence of many witnesses. 13 In the sight of God, who gives life to everything, and of Christ Jesus, who while testifying before Pontius Pilate(Z) made the good confession,(AA) I charge you(AB) 14 to keep this command without spot or blame(AC) until the appearing of our Lord Jesus Christ,(AD) 15 which God will bring about in his own time(AE)—God, the blessed(AF) and only Ruler,(AG) the King of kings and Lord of lords,(AH) 16 who alone is immortal(AI) and who lives in unapproachable light,(AJ) whom no one has seen or can see.(AK) To him be honor and might forever. Amen.(AL)

17 Command those who are rich(AM) in this present world not to be arrogant nor to put their hope in wealth,(AN) which is so uncertain, but to put their hope in God,(AO) who richly provides us with everything for our enjoyment.(AP) 18 Command them to do good, to be rich in good deeds,(AQ) and to be generous and willing to share.(AR) 19 In this way they will lay up treasure for themselves(AS) as a firm foundation for the coming age, so that they may take hold of(AT) the life that is truly life.

20 Timothy, guard what has been entrusted(AU) to your care. Turn away from godless chatter(AV) and the opposing ideas of what is falsely called knowledge, 21 which some have professed and in so doing have departed from the faith.(AW)

Grace be with you all.(AX)

Footnotes

  1. 1 Timothy 6:2 Or and benefit from the service