Maisha Yanayompendeza Mungu

Hatimaye, ndugu wapendwa, tuliwaelekeza namna mnavyopaswa kuishi ili kumpendeza Mungu. Na kweli ndivyo mnavyoishi. Sasa tunawaombeni na kuwasihi katika jina la Bwana Yesu, mwendelee kufanya hivyo zaidi na zaidi. Mnafahamu maelekezo tuliyowapa kwa mamlaka ya Bwana Yesu.

Mungu anapenda ninyi muwe watakatifu, mjiepushe na maisha ya zinaa; na kwamba kila mmoja wenu ajifunze kuishi na mke wake mwenyewe kwa njia ya utakatifu na heshima; si kwa kutawaliwa na tamaa mbaya kama watu wa mataifa wasiomjua Mungu. Katika jambo hili mtu asije akamkosea au kumdanganya ndugu yake. Kama tulivy okwisha kuwaambia na kuwaonya, Bwana atawaadhibu watu watendao dhambi zote za aina hii. Kwa maana Mungu hakutuita tutawaliwe na mawazo machafu, bali tuishi maisha ya utakatifu. Kwa hiyo mtu ye yote anayekataa mafundisho haya hamkatai mwanadamu bali anamkataa Mungu anayewapa ninyi Roho wake Mtakatifu.

Hatuna haja ya kuwaandikia kuhusu upendo kati ya ndugu, kwa maana ninyi wenyewe mmekwisha kufundishwa na Mungu mpendane ninyi kwa ninyi 10 na kwa kweli mnawapenda ndugu wote wa Makedonia yote. Hata hivyo, ndugu zetu, tunawasihi mwendelee kuwapenda zaidi sana. 11 Jitahidini kuishi maisha ya utulivu, kila mtu akishughulikia mambo yake mwenyewe na kufanya kazi kwa mikono yenu, kama tulivyowaambia. 12 Kwa njia hii maisha yenu ya kila siku yatawaletea sifa kutoka kwa watu wasioamini na wala hamtahi taji kuwategemea watu wengine.

Kufufuliwa Kwa Wafu Na Kuja Kwa Bwana

13 Ndugu wapendwa, hatupendi mkose kujua kuhusu wale wanaokufa, au mhuzunike kama watu wasiokuwa na tumaini. 14 Tunaamini kwamba Yesu alikufa na kufufuka, kwa hiyo tunaamini kwamba Mungu atawainua wale waliokufa pamoja na Kristo wakiwa ndani yake. 15 Kama alivyosema Bwana mwenyewe, tunawaambieni kuwa sisi ambao tuko hai bado, tutakaokuwa hai mpaka Bwana arudi, kwa hakika hatutawatangulia wale waliokwisha kufa.

16 Kwa maana Bwana mwenyewe atashuka toka mbinguni, akitoa amri kwa sauti kuu pamoja na sauti ya malaika mkuu na sauti ya tarumbeta ya Mungu; na wale waliokufa wakiwa wanamwamini Kristo watafufuka kwanza. 17 Kisha sisi tulio hai bado, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu tukutane na Bwana angani. Na hivyo tutakuwa na Bwana milele. 18 Kwa hiyo farijianeni kwa maneno haya.

Living to Please God

As for other matters, brothers and sisters,(A) we instructed you how to live(B) in order to please God,(C) as in fact you are living. Now we ask you and urge you in the Lord Jesus to do this more and more. For you know what instructions we gave you by the authority of the Lord Jesus.

It is God’s will(D) that you should be sanctified: that you should avoid sexual immorality;(E) that each of you should learn to control your own body[a](F) in a way that is holy and honorable, not in passionate lust(G) like the pagans,(H) who do not know God;(I) and that in this matter no one should wrong or take advantage of a brother or sister.[b](J) The Lord will punish(K) all those who commit such sins,(L) as we told you and warned you before. For God did not call us to be impure, but to live a holy life.(M) Therefore, anyone who rejects this instruction does not reject a human being but God, the very God who gives you his Holy Spirit.(N)

Now about your love for one another(O) we do not need to write to you,(P) for you yourselves have been taught by God(Q) to love each other.(R) 10 And in fact, you do love all of God’s family throughout Macedonia.(S) Yet we urge you, brothers and sisters, to do so more and more,(T) 11 and to make it your ambition to lead a quiet life: You should mind your own business and work with your hands,(U) just as we told you, 12 so that your daily life may win the respect of outsiders(V) and so that you will not be dependent on anybody.

Believers Who Have Died

13 Brothers and sisters, we do not want you to be uninformed(W) about those who sleep in death,(X) so that you do not grieve like the rest of mankind, who have no hope.(Y) 14 For we believe that Jesus died and rose again,(Z) and so we believe that God will bring with Jesus those who have fallen asleep in him.(AA) 15 According to the Lord’s word, we tell you that we who are still alive, who are left until the coming of the Lord,(AB) will certainly not precede those who have fallen asleep.(AC) 16 For the Lord himself will come down from heaven,(AD) with a loud command, with the voice of the archangel(AE) and with the trumpet call of God,(AF) and the dead in Christ will rise first.(AG) 17 After that, we who are still alive and are left(AH) will be caught up together with them in the clouds(AI) to meet the Lord in the air. And so we will be with the Lord(AJ) forever. 18 Therefore encourage one another(AK) with these words.

Footnotes

  1. 1 Thessalonians 4:4 Or learn to live with your own wife; or learn to acquire a wife
  2. 1 Thessalonians 4:6 The Greek word for brother or sister (adelphos) refers here to a believer, whether man or woman, as part of God’s family.