Maono Ya Paulo Na Mwiba Aliokuwa Nao

12 Inanibidi nijisifu. Ingawa hakuna faida, nitawaeleza juu ya maono na mafunuo niliyopata kutoka kwa Bwana. Namfahamu mtu aliyekuwa ndani ya Kristo ambaye miaka kumi na minne iliyopita alijikuta katika mbingu ya tatu. Kama alikuwa katika mwili au katika roho mimi sijui, Mungu anajua. Na ninafahamu ya kuwa huyu mtu alijikuta yuko Paradiso, kama alikuwa katika mwili au katika roho mimi sijui, Mungu anajua. Naye alisikia mambo ambayo hayawezi kusimuliwa, ambayo mtu hawezi kuyatamka. Kwa niaba ya mtu huyu nitajisifu, lakini kwa ajili yangu mwenyewe sitajisifu isipokuwa kuhusu udhaifu wangu. Lakini ningependa kujisifu, sitakuwa mjinga kwa maana nitakuwa nasema kweli. Ila najizuia, ili mtu ye yote asije akaniona mimi kuwa bora zaidi kuliko ninavyoonekana katika yale ninayotenda na kusema.

Na ili nisijione bora kuliko nilivyo, kutokana na mafunuo haya makuu, nilipewa mwiba katika mwili wangu, mtumishi wa she tani, ili anitese. Nimemsihi Bwana mara tatu aniondolee mwiba huu. Lakini aliniambia, “Neema yangu inakutosha, kwa kuwa uwezo wangu unakamilika katika udhaifu.” Kwa hiyo nitajisifu kwa furaha zaidi kuhusu udhaifu wangu ili uwezo wa Kristo ukae juu yangu. 10 Basi, kwa ajili ya Kristo, naridhika na udhaifu, mat usi, taabu, mateso na maafa; kwa maana ninapokuwa mdhaifu ndipo nina nguvu.

Upendo Wa Paulo Kwa Wakorintho

11 Nimekuwa mjinga, lakini ninyi mmenilazimisha niwe hivyo. Kwa kuwa ninyi ndio ambao mngenisifu. Kwa sababu sikuwa wa chini kuliko hawa “mitume wakuu,” hata ingawa mimi si kitu. 12 Mambo yanayomtambulisha mtume wa kweli, yaani ishara, miujiza na maaj abu, yalifanywa miongoni mwenu kwa uvumilivu wote. 13 Je, kuna kitu ambacho hamkupewa sawa na wengine, isipokuwa mimi sikuwa mzigo kwenu? Nisameheni kwa kosa hili.

14 Na sasa niko tayari kuwatembelea kwa mara ya tatu, nami sitahitaji msaada wenu kwa sababu sitaki mnipe mali yenu, ninaowahitaji ni ninyi. Kwa kuwa si sawa watoto waweke akiba kwa ajili ya wazazi wao bali wazazi waweke akiba kwa ajili ya watoto wao. 15 Nitafurahi kutumia kila nilicho nacho hata mwili wangu pia, kwa ajili yenu. Je kama nawapenda zaidi, mtanipenda kidogo tu kwa sababu hiyo? 16 Hata kama mnakubali kwamba sikuwa mzigo kwenu, wengine watasema nilikuwa mjanja nikawanasa kwa hila. 17 Je, niliwahi kuwadanganya kupitia mmojawapo wa hao watu nil iowatuma kwenu? 18 Nilimsihi Tito aje kwenu nikamtuma ndugu mwingine waje pamoja. Je, Tito aliwatoza cho chote? Je, sisi sote hatukutenda kwa kuongozwa na Roho mmoja na kufuata njia moja?

19 Pengine mnafikiri wakati wote kwamba sisi tunajaribu kujitetea mbele yenu. Sisi tunajitetea mbele ya Mungu katika Kristo, na yote haya ni kwa nia ya kuwajenga ninyi, wapendwa wetu. 20 Kwa maana nina hofu kwamba nitakapokuja nitawakuta hamko kama ambavyo ningependa muwe, na ninyi mtakuta siko kama ambavyo mngependa niwe. Nina hofu kwamba kati yenu huenda kuna ugomvi, wivu, hasira, ubinafsi, uzushi, usengenyaji, majivuno na machafuko. 21 Nina hofu kuwa nitakapokuja tena Mungu wangu ata ninyenyekeza mbele yenu, na huenda nikaomboleza kuhusu wengi wenu ambao walitenda dhambi na hawajatubu na kuacha hayo matendo machafu, uasherati na ufisadi ambao walikuwa wakitenda.

Nguvu ya Paulo Inatoka Katika Udhaifu

12 Inanipasa kuendelea kujivuna juu yangu mwenyewe. Hiyo haitasaidia, lakini nitazungumza juu ya maono na mafunuo kutoka kwa Bwana. Ninamjua mtu mmoja[a] katika Kristo aliyechukuliwa juu katika mbingu ya tatu. Hili lilitokea miaka 14 iliyopita. Sifahamu ikiwa mtu huyu alikuwa ndani ya mwili wake au nje ya mwili wake, lakini Mungu anajua. 3-4 Na ninajua kuwa mtu huyu alichukuliwa juu paradiso. Sijui kama alikuwa katika mwili wake au nje ya mwili wake. Mungu pekee ndiye anajua. Lakini mtu huyu aliyasikia mambo ambayo hana uwezo wa kuyasimulia. Alisikia mambo ambayo mtu yeyote anaruhusiwa kuyasema. Nitajivunia mtu wa namna hiyo, lakini sitajivuna juu yangu mwenyewe. Nitajivuna tu katika madhaifu yangu.

Lakini ikiwa nilitaka kujivuna, sitakuwa nikizungumza kama mjinga, kwa sababu ningekuwa nasema iliyo kweli. Lakini sitajivuna tena zaidi, kwa sababu sitaki watu wanifikirie kwa ubora zaidi kuliko wanavyoniona nikitenda ama kusikia ninayosema.

Lakini imenipasa kutojivuna zaidi juu ya mambo ya ajabu yaliyoonyeshwa kwangu. Kwa sababu hiyo nilipewa tatizo lenye maumivu;[b] malaika toka kwa Shetani; aliyetumwa kwangu kunitesa, ili nisiweze kufikiri kwamba mimi ni bora zaidi kuliko watu wengine. Nilimwomba Bwana mara tatu kuliondoa tatizo hili kwangu. Lakini Bwana alisema, “Neema yangu ndiyo unayoihitaji. Ni pale tu unapokuwa dhaifu ndipo kila kitu kinapoweza kufanyika katika uwezo wangu.” Hivyo nitajivunia udhaifu wangu kwa furaha. Hapo ndipo uweza wa Kristo unaweza kukaa ndani yangu. 10 Ndiyo, nina furaha kuwa na madhaifu ikiwa ni kwa ajili ya Kristo. Nina furaha kuaibishwa na kupitia magumu. Nina furaha ninapoteswa na kupata matatizo, kwa sababu ni pale nilipodhaifu ndipo ninapokuwa na nguvu.

Upendo wa Paulo kwa Waamini wa Korintho

11 Nimekuwa nikizungumza kama mjinga, lakini ninyi ndiyo mliosababisha nikafanya hivyo. Ninyi ndiyo mnaopaswa kuzungumza mema juu yangu. Mimi si kitu, lakini mimi si myonge kwa njia yeyote ile kwa hao “mitume wakuu”. 12 Nilipokuwa pamoja nanyi, nilifanya kwa uvumilivu wote vitu vilivyo nilidhihirisha kuwa mimi ni mtume kwa ishara, maajabu na miujiza. 13 Kwa hiyo mlipokea kila kitu ambacho makanisa yote yalipata. Kitu kimoja tu ndicho kilikuwa cha tofauti na cha kipekee: Sikuwa mzigo au msumbufu kwenu. Mnisamehe kwa hilo.

14 Niko tayari sasa kuwatembelea kwa mara ya tatu, na sitakuwa mzigo kwenu. Mimi sitafuti kitu chochote kilicho chenu. Ninawataka ninyi tu. Watoto wasiweke akiba vitu vya kuwapa wazazi wao. Wazazi wanapaswa kuweka akiba vitu vya kuwapa watoto wao. 15 Kwa hiyo ninayo furaha kutumia kile nilichonacho kwa ajili yenu. Na mimi mwenyewe nitajitoa kikamilifu kwa ajili yenu. Je, kama upendo wangu kwenu utakuwa mkubwa, upendo wenu kwangu utapungua?

16 Ni wazi kuwa sikuwa mzigo kwenu, lakini baadhi yenu wanadhani kuwa nilikuwa mjanja, na kutumia hila kuwaweka mtegoni. 17 Je, niliwadanganya kwa kuwatumia mtu yeyote kati ya wale niliyowatuma kwenu? Mnafahamu kuwa sikufanya hivyo. 18 Nilimwomba Tito aje kwenu, na nilimtuma kaka yetu afuatane naye. Tito hakuwadanganya, je alifanya hivyo? Hapana! Na kwa hiyo mjue kuwa matendo yangu na tabia yangu ilikuwa ya dhati kama ilivyokuwa kwake.

19 Je! Mnadhani tumekuwa tukijitetea? Hapana, tunasema haya katika Kristo na mbele za Mungu. Ninyi ni rafiki zetu wapendwa, na kila tunachofanya tunakifanya ili muwe imara. 20 Ninafanya hivi kwa sababu ninaogopa kuwa nitakapokuja, hamtakuwa kama vile ninavyotaka muwe. Na pia nina wasiwasi kuwa sitakuwa kwa namna ile mnayotaka mimi niwe. Nina hofu kuwa nitawakuta mkibishana, wenye wivu, wenye hasira, mkipigana kwa ubinafsi wenu, wenye misemo mibaya, watetaji, wenye kiburi, na machafuko huko. 21 Nina wasiwasi kuwa nitakapokuja kwenu, Mungu wangu ataninyenyekeza tena mbele yenu. Nitalazimika kuomboleza kwa ajili ya wale ambao wametenda dhambi. Wengi wao hawajarejea na kutubia maisha yao ya uovu, dhambi za zinaa, na mambo ya aibu waliyotenda.

Footnotes

  1. 12:2 mtu mmoja Katika sura 12:2-5 Paulo huenda anasema habari zake mwenyewe.
  2. 12:7 tatizo lenye maumivu Kwa maana ya kawaida, “mwiba mwilini”.