Kuja Kwa Bwana Na Kudhihirishwa Kwa Mwovu

Basi, kuhusu kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanyika kwetu mbele zake, tunawasihi, ndugu wapendwa, msifadhaike au kuwa na wasiwasi kutokana na utabiri fulani, au taarifa au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu, kusema eti kwamba siku ya Bwana imekwisha kuja. Mtu asiwadanganye kwa namna yo yote maana siku hiyo haitakuja kabla ya uasi kutokea kwanza na yule mwasi adhi hirishwe, yule ambaye mwisho wake ni kuangamizwa kabisa. Yeye anapinga kila ambacho watu hukiita mungu au cho chote kinachoabu diwa; naye hujiweka hata katika Hekalu la Mungu, akijitangaza mwenyewe kuwa ndiye Mungu.

Je, hamkumbuki kuwa nilipokuwa pamoja nanyi niliwaambieni mambo haya? Na mnajua kinachomzuia sasa, ili adhihirishwe wakati ufaao. Maana ile nguvu ya siri ya uasi imekwisha anza kufanya kazi; lakini yule anayeizuia ataendelea kufanya hivyo mpaka atakapoondolewa. Hapo ndipo yule mwovu ataonekana, na Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kabisa kwa ufahari wa kuja kwake. Kuja kwa yule mwovu kutafuata kazi ya shetani ambayo itaonyeshwa katika aina zote za ishara bandia na maajabu ya uongo; 10 na katika kila aina ya uovu unaotumiwa kuwadanganya wale wanaoangamia. Wanaangamia kwa sababu walikataa kuipenda kweli wapate kuokolewa. 11 Ndio maana Mungu ameruhusu watawaliwe na nguvu ya udanganyifu ili waendelee kuu amini uongo; 12 na ili wote wasioamini kweli bali hufurahia uovu, wahukumiwe.

Simameni Imara

13 Lakini tunapaswa kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu, ndugu mpendwao na Bwana, maana Mungu aliwachagueni tangu mwanzo ili mwokolewe kwa kutakaswa na Roho na kwa kuiamini kweli. 14 Mungu amewaitieni jambo hili kwa njia ya mahubiri yetu ya Habari Njema, ili muweze kushiriki katika utukufu wa Bwana Yesu Kristo. 15 Kwa hiyo ndugu wapendwa, simameni imara na mshike sana yale mafundisho tuliyowapeni katika mahubiri yetu na kwa barua zetu.

16 Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, ali yetupenda akatupatia faraja ya milele na tumaini jema kwa neema, 17 na awafariji mioyoni mwenu na kuwaimarisheni katika kila jambo jema mnalosema au kutenda.

Mambo Maovu Yatatokea

Kaka na dada, tuna jambo la kuwaambia juu ya kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Tunataka kuzungumza nanyi juu ya wakati huo tutakapokusanyika pamoja naye. Msikubali kufadhaishwa na kutiwa kuhofu ikiwa mtasikia kwamba siku ya Bwana tayari imekwishawadia. Wengine wanaweza kusema kwamba wazo hili limetoka kwetu katika jambo alilotuambia Roho, au tulilosema, au katika barua tuliyoiandika. Msidanganywe na chochote wanachoweza kusema kuhusu kuja kwa Bwana. Siku hiyo ya Bwana haitakuja mpaka itanguliwe na kukengeuka kwa wanadamu na kumwacha Mungu. Na siku hiyo haitakuja mpaka ajitokeze kwanza Mtu wa Uovu, yule ambaye ana uhakika kuwa ataangamizwa.[a] Huyo atasimama kinyume na kujiweka mwenyewe juu ya kila kitu ambacho watu wanaabudu au kudhani kuwa kinafaa kuabudiwa. Ataenda na kuingia ndani ya Hekalu[b] na kukikalia kiti cha enzi, akidai kuwa yeye ni Mungu.

Niliwaambia zaidi ya mara moja nilipokuwa huko kwamba mambo yote haya yangetokea. Je, mnakumbuka? Na mnafahamu kinachomzuia Mtu wa Uovu. Huyo hataruhusiwa kuonekana mpaka wakati sahihi utakapofika. Tayari nguvu ya uovu inatenda kazi ulimwenguni sasa. Lakini yupo mmoja anayeizuia nguvu hiyo. Na ataendelea kuizuia mpaka atakapoondolewa. Kisha huyo Mtu wa Uovu atatokea. Lakini Bwana Yesu atamuua kwa pumzi inayotoka katika kinywa chake. Bwana atakuja katika namna ambayo kila mtu atamwona, na huo utakuwa mwisho wa Mtu wa Uovu.

Kuja kwa Mtu wa Uovu itakuwa kazi ya Shetani. Atakuja na nguvu kuu, na atafanya aina zote za miujiza ya uongo, ishara, na maajabu. 10 Mtu wa Uovu atatumia kila aina ya uovu kuwatia ujinga wote walio njiani kuelekea kuangamia. Wamepotea kwa sababu walikataa kuupenda ujumbe wenye ukweli kuhusu Yesu na kuokolewa. 11 Hivyo Mungu atawaacha wadanganyike hata kuamini uongo.[c] 12 Wote watahukumiwa kwa sababu hawakuamini ujumbe wa kweli na kwa kuwa walifurahia kufanya maovu.

Mmechaguliwa kwa ajili ya Wokovu

13 Ndugu zangu, ninyi ni watu mnaopendwa na Bwana. Na imetupasa tumshukuru Mungu daima kwa sababu yenu. Hayo ndiyo tunayotakiwa kuyatenda, kwa sababu Mungu aliwaita kuwa miongoni mwa watu[d] wa kwanza kuokolewa. Mmeokolewa na Roho aliyewafanya muwe watu wa Mungu walio watakatifu kupitia kuiamini kweli. 14 Mungu aliwaita ninyi mpate wokovu. Aliwaita kwa kutumia Habari Njema tuliwahubiri. Mliitwa ili mshiriki katika utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo. 15 Hivyo simameni imara na kuendelea kuamini mafundisho tuliyowapa tulipokuwa huko na kupitia barua yetu.

16-17 Tunaomba kwamba Bwana Yesu Kristo na Mungu Baba yetu awafariji na kuwaimairisha katika kila jambo jema mnalotenda na kusema. Mungu alitupenda na kutupa kupitia neema matumaini ya ajabu na faraja isiyo na mwisho.

Footnotes

  1. 2:3 ataangamizwa Au “Kusababisha uharibifu”. Kwa maana ya kawaida, “ni mwana wa uharibifu”.
  2. 2:4 Hekalu Pengine Hekalu katika Yerusalemu. Tazama Hekalu katika Orodha ya Maneno.
  3. 2:11 uongo Ina maana ya kuamini uongo (mkubwa) juu ya Muasi (ya kwamba Muasi ndiye Mungu).
  4. 2:13 kuwa … watu Nakala zingine za Kiyunani zimeongeza, “kuanzia mwanzo”.

The Man of Lawlessness

Concerning the coming of our Lord Jesus Christ(A) and our being gathered to him,(B) we ask you, brothers and sisters, not to become easily unsettled or alarmed by the teaching allegedly from us—whether by a prophecy or by word of mouth or by letter(C)—asserting that the day of the Lord(D) has already come.(E) Don’t let anyone deceive you(F) in any way, for that day will not come until the rebellion(G) occurs and the man of lawlessness[a] is revealed,(H) the man doomed to destruction. He will oppose and will exalt himself over everything that is called God(I) or is worshiped, so that he sets himself up in God’s temple, proclaiming himself to be God.(J)

Don’t you remember that when I was with you I used to tell you these things?(K) And now you know what is holding him back,(L) so that he may be revealed at the proper time. For the secret power of lawlessness is already at work; but the one who now holds it back(M) will continue to do so till he is taken out of the way. And then the lawless one will be revealed,(N) whom the Lord Jesus will overthrow with the breath of his mouth(O) and destroy by the splendor of his coming.(P) The coming of the lawless one will be in accordance with how Satan(Q) works. He will use all sorts of displays of power through signs and wonders(R) that serve the lie, 10 and all the ways that wickedness deceives those who are perishing.(S) They perish because they refused to love the truth and so be saved.(T) 11 For this reason God sends them(U) a powerful delusion(V) so that they will believe the lie(W) 12 and so that all will be condemned who have not believed the truth but have delighted in wickedness.(X)

Stand Firm

13 But we ought always to thank God for you,(Y) brothers and sisters loved by the Lord, because God chose you as firstfruits[b](Z) to be saved(AA) through the sanctifying work of the Spirit(AB) and through belief in the truth. 14 He called you(AC) to this through our gospel,(AD) that you might share in the glory of our Lord Jesus Christ.

15 So then, brothers and sisters, stand firm(AE) and hold fast to the teachings[c] we passed on to you,(AF) whether by word of mouth or by letter.

16 May our Lord Jesus Christ himself and God our Father,(AG) who loved us(AH) and by his grace gave us eternal encouragement and good hope, 17 encourage(AI) your hearts and strengthen(AJ) you in every good deed and word.

Footnotes

  1. 2 Thessalonians 2:3 Some manuscripts sin
  2. 2 Thessalonians 2:13 Some manuscripts because from the beginning God chose you
  3. 2 Thessalonians 2:15 Or traditions