Font Size
Luka 18:31-34
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Luka 18:31-34
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Azungumza Tena Kuhusu Kifo Chake
(Mt 20:17-19; Mk 10:32-34)
31 Kisha Yesu alizungumza na mitume wake kumi na mbili wakiwa peke yao. Akawaaambia, “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu. Kila kitu ambacho Mungu aliwaambia manabii waandike kuhusu Mwana wa Adamu kitatokea. 32 Atakabidhiwa kwa wasio Wayahudi, ambao watamcheka, watamtukana na kumtemea mate. 33 Watamchapa kwa mijeledi kisha watamuua. Lakini katika siku ya tatu baada ya kifo chake, atafufuka kutoka kwa wafu.” 34 Mitume walijaribu kulielewa hili, lakini hawakuweza; maana yake ilifichwa wasiielewe.
Read full chapter
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi (TKU)
Copyright © 2017 by Bible League International