Marko 16:1-8
Neno: Bibilia Takatifu
Yesu Afufuka Kutoka Kwa Wafu
16 Sabato ilipomalizika, Mariamu Magdalena na Mariamu mama yake Yakobo na Salome walinunua manukato ili wakaupake mwili wa Yesu. 2 Asubuhi na mapema, siku ya Jumapili, walikwenda kaburini jua likiwa linaanza kuchomoza. 3 Njiani wakawa wanaulizana, “Ni nani atatuondolea lile jiwe kwenye mlango wa kaburi?” 4 Lakini walipotazama, wakaona jiwe lile, ambalo lilikuwa kubwa sana, limekwisha ondolewa.
5 Walipoingia kaburini, walimwona kijana amekaa upande wa kulia akiwa amevaa vazi jeupe. Wakashtuka. 6 Yule mtu akawaambia, “Msishtuke. Mnamtafuta Yesu Mnazareti, aliyesulubiwa. Amefufuka! Hayuko hapa! Tazameni mahali alipokuwa amelazwa.
7 Lakini nendeni mkawaambie wanafunzi wake, na Petro, kwamba anatangulia kwenda Galilaya na huko mtamwona, kama alivyowaam bia.” 8 Wale wanawake wakiwa wanashangaa na kutetemeka kwa hofu, wakatoka pale kaburini mbio! Hawakumweleza mtu ye yote jambo lo lote kwa maana walikuwa wanaogopa.
Read full chapterCopyright © 1989 by Biblica