Marko 16:1-8
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi
Yesu Amefufuka Kutoka Mauti
(Mt 28:1-8; Lk 24:1-12; Yh 20:1-10)
16 Sabato ilipomalizika, Mariamu Magdalena, Maria mama yake Yakobo, na Salome wakanunua manukato yenye harufu nzuri ili kuyapaka kwenye mwili wa Yesu. 2 Alfajiri na mapema Jumapili, mara tu baada ya jua kuchomoza, walienda kwenye kaburi la Yesu. 3 Nao walikuwa wakiambiana wao kwa wao, ni nani atakayelivingirisha jiwe litoke katika mlango wa kaburi kwa ajili yetu?
4 Kisha wakatazama juu na wakaona kuwa jiwe lile kubwa lilikuwa limevingirishwa tayari litoke mlangoni mwa kaburi la Yesu. 5 Walipoingia kaburini, wakamwona kijana mmoja ameketi upande wa kulia naye alikuwa amevaa vazi jeupe, nao wakastaajabu.
6 Naye akamwambia, “Usistaajabu. Unamtafuta Yesu wa Nazareti, aliyesulubiwa? Tazama amefufuka! Hayupo hapa. Angalieni mahali walipokuwa wameweka mwili wake. 7 Hata hivyo nendeni na kuwaeleza wafuasi wake pamoja na Petro kwamba: ‘Ametangulia mbele yenu kuelekea Galilaya. Mtamkuta kule, kama alivyowaambia.’”
8 Kwa hiyo wale wanawake walitoka na kukimbia kutoka kaburini, kwa sababu hofu na mshangao ulikuwa umewajia. Nao hawakusema chochote kwa mtu yeyote kwani waliogopa.[a]
Read full chapterFootnotes
- 16:8 Kitabu kinaishia hapa katika nakala mbili za zamani za Kiyunani zilizopatikana. Nakala chache nyingine za baadaye zina mwisho huu mfupi: “Lakini mara wakampa maagizo yote Petro na wale waliokuwa pamoja naye. Kisha Yesu mwenyewe akawatuma watoke na kwenda mashariki na magharibi wakiwa na ujumbe mtakatifu ambao kamwe hautabadilika; kwamba watu wataokolewa milele.”
Marko 16:1-8
Neno: Bibilia Takatifu
Yesu Afufuka Kutoka Kwa Wafu
16 Sabato ilipomalizika, Mariamu Magdalena na Mariamu mama yake Yakobo na Salome walinunua manukato ili wakaupake mwili wa Yesu. 2 Asubuhi na mapema, siku ya Jumapili, walikwenda kaburini jua likiwa linaanza kuchomoza. 3 Njiani wakawa wanaulizana, “Ni nani atatuondolea lile jiwe kwenye mlango wa kaburi?” 4 Lakini walipotazama, wakaona jiwe lile, ambalo lilikuwa kubwa sana, limekwisha ondolewa.
5 Walipoingia kaburini, walimwona kijana amekaa upande wa kulia akiwa amevaa vazi jeupe. Wakashtuka. 6 Yule mtu akawaambia, “Msishtuke. Mnamtafuta Yesu Mnazareti, aliyesulubiwa. Amefufuka! Hayuko hapa! Tazameni mahali alipokuwa amelazwa.
7 Lakini nendeni mkawaambie wanafunzi wake, na Petro, kwamba anatangulia kwenda Galilaya na huko mtamwona, kama alivyowaam bia.” 8 Wale wanawake wakiwa wanashangaa na kutetemeka kwa hofu, wakatoka pale kaburini mbio! Hawakumweleza mtu ye yote jambo lo lote kwa maana walikuwa wanaogopa.
Read full chapterCopyright © 2017 by Bible League International
Copyright © 1989 by Biblica