Mpango Wa Kumwua Yesu

14 Siku mbili tu kabla ya sikukuu ya Pasaka na sherehe ya mikate isiyotiwa chachu, makuhani wakuu na walimu wa sheria wali kuwa wakitafuta njia ya kumkamata Yesu kwa siri na kumwua. Wakaambiana, “Jambo hili tusilifanye wakati wa sikukuu maana watu wanaweza kufanya ghasia.”

Yesu Apakwa Manukato

Yesu alikuwa Bethania nyumbani kwa Simoni ambaye aliwahi kuwa na ukoma. Alipokuwa mezani akila chakula cha jioni, mwanamke mmoja aliingia ndani akiwa na chupa ya alabasta yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa. Akaivunja hiyo chupa, akammiminia Yesu manukato hayo kichwani. Baadhi ya watu waliokuwapo wali chukia wakasema, “Kwa nini anapoteza bure manukato hayo? Si afadhali yangeliuzwa kwa dinari zaidi ya mia tatu na fedha hizo wakapewa maskini?” Wakamkemea huyo mama kwa hasira. Lakini Yesu akawaambia, “Kwa nini mnamnyanyasa? Mwacheni! Amenitendea jambo zuri na jema. Maskini mnao wakati wote na mnaweza kuwapa tia msaada wakati wo wote mtakapo. Lakini hamtakuwa nami wakati wote. Huyu mama amenitendea lile aliloweza. Amenipaka manukato kuniandaa kwa mazishi yangu. Nawaambieni hakika, mahali po pote duniani ambapo Habari Njema itahubiriwa, jambo hili alilo nitendea huyu mama, litatajwa kwa ukumbusho wake.”

Yuda Anapanga Kumsaliti Yesu

10 Kisha Yuda Iskariote, mmoja wa wale wanafunzi kumi na wawili, akaenda kwa makuhani wakuu kuwaambia kuwa yuko tayari kuwasaidia wamkamate Yesu. 11 Walifurahishwa sana na habari hizi, wakaahidi kumlipa fedha. Kwa hiyo yeye akaanza kutafuta nafasi nzuri ya kumsaliti.

Yesu Anakula Pasaka Na Wanafunzi Wake

12 Siku ya kwanza ya sherehe ya Mikate isiyotiwa chachu siku ambayo kondoo wa Pasaka huchinjwa, wanafunzi wake walimwuliza Yesu, “Unapenda tukuandalie wapi chakula cha Pasaka?” 13 Aka watuma wanafunzi wawili akawaagiza, “Nendeni mjini. Huko mtaku tana na mwanamume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni, 14 na pale atakapoingia, mwambieni mwenye nyumba, ‘Mwalimu anasema hivi, kiko wapi chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?’ 15 Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani kilichopangwa tayari. Tuandalieni humo.” 16 Wale wanafunzi walikwenda mjini wakakuta kila kitu kama alivyowaambia; wakaandaa chakula cha Pasaka. 17 Ilipofika jioni, Yesu akaja pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili. 18 Walipokuwa mezani wakila, akawaambia, “Ninawaam bia hakika, mmoja wenu anayekula pamoja nami, atanisaliti.” 19 Wote wakasikitika. Wakamwuliza mmoja mmoja, “Ni mimi, Bwana?” 20 Akawajibu, “Ni mmoja wenu kumi na wawili, yule anayechovya kipande chake cha mkate kwenye bakuli pamoja nami. 21 Mimi Mwana wa Adamu sina budi kufa kama maandiko yasemavyo. Lakini ole wake yeye atakayenisaliti. Ingelikuwa heri kama hakuz aliwa!”

Chakula Cha Bwana

22 Walipokuwa wakila, Yesu akachukua mkate, akashukuru , akaumega akawapa wanafunzi wake akisema, “Pokeeni, huu ni mwili wangu.” 23 Kisha akachukua kikombe, akashukuru, akawapa, wote wakanywa humo. 24 Akawaambia, “Hii ni damu yangu ya agano, inayomwagwa kwa faida ya wengi. 25 Nawaambieni hakika, sita kunywa tena divai mpaka siku ile nitakapokunywa divai mpya katika Ufalme wa Mungu.”

26 Walipokwisha kuimba wimbo walikwenda kwenye mlima wa

Yesu Atabiri Kuwa Petro Atamkana

28 Yesu akawaambia, “Ninyi nyote mtakimbia mniache kwa maana imeandikwa: ‘Nitampiga mchungaji na kondoo watatawanyika.’ 29 Lakini nikisha fufuka nitawatangulia kwenda Galilaya. 30 Petro akasema, “Hata kama wengine wote watakuacha, mimi sitakuacha.” Yesu akamwambia, “Ninakwambia hakika, usiku huu huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, utakanusha mara tatu kwamba hunifahamu.” 31 Lakini Petro akasisitiza, “Hata kama ni lazima niuawe pamoja nawe, sitakukana.” Na wale wanafunzi wen gine wote wakasema hivyo hivyo.

Yesu Anasali Bustanini Gethsemane

32 Wakafika mahali paitwapo Gethsemane, Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa wakati mimi naomba.” 33 Kisha aka wachukua Petro na Yakobo na Yohana. Akawa na huzuni na uchungu mwingi. 34 Akawaambia, “Moyo wangu umejaa huzuni kiasi cha kufa; kaeni hapa mkeshe.” 35 Akaenda mbele kidogo, akajitupa chi ni akaomba kuwa kama ikiwezekana saa hiyo ya mateso aiepuke. 36 Akasema, “Aba, Baba, mambo yote yawezekana kwako. Tafadhali niondolee kikombe hiki cha mateso. Lakini si kama nitakavyo mimi, bali mapenzi yako yatimizwe.” 37 Akarudi, akakuta wame lala. Akamwambia Petro, “Simoni, umelala? Hukuweza kukesha hata kwa saa moja? 38 Kesheni na kuomba msije mkaingia katika majar ibu. Roho i radhi lakini mwili ni dhaifu.” 39 Akaondoka tena akaenda kuomba akisema maneno yale yale. 40 Aliporudi tena ali wakuta wanafunzi wake wamelala; macho yao yalikuwa mazito na hawakujua la kumwambia. 41 Aliporudi mara ya tatu aliwaambia, “ Bado mmelala na kupumzika? Imetosha! Saa imefika. Mimi Mwana wa Adamu ninatiwa mikononi mwa wenye dhambi. 42 Amkeni twendeni, tazameni, yule ambaye amenisaliti amekaribia.”

Yesu Akamatwa

43 Yesu alipokuwa bado anazungumza, Yuda, mmoja wa wale wanafunzi kumi na wawili, akafika pamoja na umati wa watu wenye mapanga na marungu. Watu hao walikuwa wametumwa na makuhani wakuu, waandishi, na wazee. 44 Yuda, yule msaliti, alikuwa amewapa ishara wale watu kuwa, “Yule nitakayembusu, ndiye mnayemtaka, mkamateni na kumchukua akiwa chini ya ulinzi.”

45 Kwa hiyo Yuda alipofika, alimwendea Yesu akamwambia, “Mwalimu,” akambusu. 46 Wakamkamata Yesu, wakamweka chini ya ulinzi. 47 Lakini mmoja wa wale waliokuwa wamesimama hapo aka chukua upanga akampiga mtumishi wa kuhani mkuu, akamkata sikio. 48 Kisha Yesu akasema, “Mbona mmekuja kunikamata kwa mapanga na marungu? Kwani mimi ni jambazi? 49 Siku zote nilikuwa pamoja nanyi nikifundisha Hekaluni wala hamkunikamata. Lakini Maandiko lazima yatimie. ” 50 Ndipo wanafunzi wake wote wakamwacha, wakakimbia. 51 Kijana mmoja aliyekuwa amevaa shuka tu alikuwa akimfuata Yesu. Walipomkamata, 52 alikimbia uchi, akaacha shuka lake.

Yesu Afikishwa Barazani

53 Kisha wakampeleka Yesu nyumbani kwa kuhani mkuu ambapo makuhani wakuu, wazee, na walimu wa sheria walikuwa wamekuta nika. 54 Petro aliwafuata kwa mbali, akaingia barazani kwa kuhani mkuu, akaketi pamoja na walinzi akiota moto. 55 Makuhani wakuu na wajumbe wote wa Baraza walijaribu kutafuta ushahidi wa kumshtaki Yesu ili wapate kumwua, lakini hawakupata. 56 Wengi walitoa ushahidi wa uongo, lakini ushahidi wao haukupatana.

57 Ndipo watu fulani wakasimama wakatoa ushahidi wa uongo wakisema, 58 “Sisi tulimsikia akisema, ‘Mimi nitabomoa Hekalu hili lililojengwa na wanadamu, na katika siku tatu nitajenga lin gine ambalo halikujengwa na wanadamu.’ ” 59 Lakini hata hawa, ushahidi wao ulipingana.

60 Kuhani Mkuu akasimama mbele ya Baraza akamwuliza Yesu, “Huwezi kujibu mashtaka haya ambayo watu hawa wameleta juu yako?” 61 Lakini Yesu alikaa kimya; hakusema neno lo lote. Kuhani Mkuu akamwuliza, “Wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu Mtu kufu?” 62 Yesu akajibu, “Mimi ndiye, na mtaniona mimi Mwana wa Adamu nimeketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi, na nikija na mawingu ya mbinguni.”

63 Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akasema, “Tuna haja gani tena ya mashahidi? 64 Ninyi wote mmemsikia akikufuru! Mna toa hukumu gani?” Wote wakamhukumu kwamba ana hatia na auawe.

65 Kisha baadhi ya watu wakaanza kumtemea mate; wakamfunga kitambaa usoni wakampiga na kumwambia, “Toa unabii, utuambie nani amekupiga!” Maaskari wakampokea kwa mapigo.

Petro Amkana Yesu

66 Petro alikuwa bado yuko barazani. Kisha akaja mtumishi mmoja wa kike wa kuhani mkuu. 67 Alipomwona Petro akiota moto, alimtazama sana, akamwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu Mnazareti.” 68 Lakini Petro akakataa, akasema, “Sijui wala sielewi unalosema,” akaondoka akaenda mlangoni. 69 Yule mtumi shi wa kike akamwona, akawaambia tena wale waliokuwa wamesimama pale, “Huyu mtu ni mmoja wao.” 70 Lakini Petro akakana tena. Baada ya muda kidogo wale waliokuwa wamesimama hapo pamoja naye wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana wewe pia ni Mgalilaya!” 71 Petro akaanza kulaani na kuapa, akawaambia, “Simjui huyo mtu mnayemsema.”

72 Hapo hapo jogoo akawika mara ya pili. Petro akakumbuka lile neno ambalo Yesu alikuwa amemwambia, “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Akalia kwa uchungu. Pilato Anamhoji Yesu

Jesus Anointed at Bethany(A)(B)(C)

14 Now the Passover(D) and the Festival of Unleavened Bread were only two days away, and the chief priests and the teachers of the law were scheming to arrest Jesus secretly and kill him.(E) “But not during the festival,” they said, “or the people may riot.”

While he was in Bethany,(F) reclining at the table in the home of Simon the Leper, a woman came with an alabaster jar of very expensive perfume, made of pure nard. She broke the jar and poured the perfume on his head.(G)

Some of those present were saying indignantly to one another, “Why this waste of perfume? It could have been sold for more than a year’s wages[a] and the money given to the poor.” And they rebuked her harshly.

“Leave her alone,” said Jesus. “Why are you bothering her? She has done a beautiful thing to me. The poor you will always have with you,[b] and you can help them any time you want.(H) But you will not always have me. She did what she could. She poured perfume on my body beforehand to prepare for my burial.(I) Truly I tell you, wherever the gospel is preached throughout the world,(J) what she has done will also be told, in memory of her.”

10 Then Judas Iscariot, one of the Twelve,(K) went to the chief priests to betray Jesus to them.(L) 11 They were delighted to hear this and promised to give him money. So he watched for an opportunity to hand him over.

The Last Supper(M)(N)

12 On the first day of the Festival of Unleavened Bread, when it was customary to sacrifice the Passover lamb,(O) Jesus’ disciples asked him, “Where do you want us to go and make preparations for you to eat the Passover?”

13 So he sent two of his disciples, telling them, “Go into the city, and a man carrying a jar of water will meet you. Follow him. 14 Say to the owner of the house he enters, ‘The Teacher asks: Where is my guest room, where I may eat the Passover with my disciples?’ 15 He will show you a large room upstairs,(P) furnished and ready. Make preparations for us there.”

16 The disciples left, went into the city and found things just as Jesus had told them. So they prepared the Passover.

17 When evening came, Jesus arrived with the Twelve. 18 While they were reclining at the table eating, he said, “Truly I tell you, one of you will betray me—one who is eating with me.”

19 They were saddened, and one by one they said to him, “Surely you don’t mean me?”

20 “It is one of the Twelve,” he replied, “one who dips bread into the bowl with me.(Q) 21 The Son of Man(R) will go just as it is written about him. But woe to that man who betrays the Son of Man! It would be better for him if he had not been born.”

22 While they were eating, Jesus took bread, and when he had given thanks, he broke it(S) and gave it to his disciples, saying, “Take it; this is my body.”

23 Then he took a cup, and when he had given thanks, he gave it to them, and they all drank from it.(T)

24 “This is my blood of the[c] covenant,(U) which is poured out for many,” he said to them. 25 “Truly I tell you, I will not drink again from the fruit of the vine until that day when I drink it new in the kingdom of God.”(V)

26 When they had sung a hymn, they went out to the Mount of Olives.(W)

Jesus Predicts Peter’s Denial(X)

27 “You will all fall away,” Jesus told them, “for it is written:

“‘I will strike the shepherd,
    and the sheep will be scattered.’[d](Y)

28 But after I have risen, I will go ahead of you into Galilee.”(Z)

29 Peter declared, “Even if all fall away, I will not.”

30 “Truly I tell you,” Jesus answered, “today—yes, tonight—before the rooster crows twice[e] you yourself will disown me three times.”(AA)

31 But Peter insisted emphatically, “Even if I have to die with you,(AB) I will never disown you.” And all the others said the same.

Gethsemane(AC)

32 They went to a place called Gethsemane, and Jesus said to his disciples, “Sit here while I pray.” 33 He took Peter, James and John(AD) along with him, and he began to be deeply distressed and troubled. 34 “My soul is overwhelmed with sorrow to the point of death,”(AE) he said to them. “Stay here and keep watch.”

35 Going a little farther, he fell to the ground and prayed that if possible the hour(AF) might pass from him. 36 “Abba,[f] Father,”(AG) he said, “everything is possible for you. Take this cup(AH) from me. Yet not what I will, but what you will.”(AI)

37 Then he returned to his disciples and found them sleeping. “Simon,” he said to Peter, “are you asleep? Couldn’t you keep watch for one hour? 38 Watch and pray so that you will not fall into temptation.(AJ) The spirit is willing, but the flesh is weak.”(AK)

39 Once more he went away and prayed the same thing. 40 When he came back, he again found them sleeping, because their eyes were heavy. They did not know what to say to him.

41 Returning the third time, he said to them, “Are you still sleeping and resting? Enough! The hour(AL) has come. Look, the Son of Man is delivered into the hands of sinners. 42 Rise! Let us go! Here comes my betrayer!”

Jesus Arrested(AM)

43 Just as he was speaking, Judas,(AN) one of the Twelve, appeared. With him was a crowd armed with swords and clubs, sent from the chief priests, the teachers of the law, and the elders.

44 Now the betrayer had arranged a signal with them: “The one I kiss is the man; arrest him and lead him away under guard.” 45 Going at once to Jesus, Judas said, “Rabbi!”(AO) and kissed him. 46 The men seized Jesus and arrested him. 47 Then one of those standing near drew his sword and struck the servant of the high priest, cutting off his ear.

48 “Am I leading a rebellion,” said Jesus, “that you have come out with swords and clubs to capture me? 49 Every day I was with you, teaching in the temple courts,(AP) and you did not arrest me. But the Scriptures must be fulfilled.”(AQ) 50 Then everyone deserted him and fled.(AR)

51 A young man, wearing nothing but a linen garment, was following Jesus. When they seized him, 52 he fled naked, leaving his garment behind.

Jesus Before the Sanhedrin(AS)(AT)

53 They took Jesus to the high priest, and all the chief priests, the elders and the teachers of the law came together. 54 Peter followed him at a distance, right into the courtyard of the high priest.(AU) There he sat with the guards and warmed himself at the fire.(AV)

55 The chief priests and the whole Sanhedrin(AW) were looking for evidence against Jesus so that they could put him to death, but they did not find any. 56 Many testified falsely against him, but their statements did not agree.

57 Then some stood up and gave this false testimony against him: 58 “We heard him say, ‘I will destroy this temple made with human hands and in three days will build another,(AX) not made with hands.’” 59 Yet even then their testimony did not agree.

60 Then the high priest stood up before them and asked Jesus, “Are you not going to answer? What is this testimony that these men are bringing against you?” 61 But Jesus remained silent and gave no answer.(AY)

Again the high priest asked him, “Are you the Messiah, the Son of the Blessed One?”(AZ)

62 “I am,” said Jesus. “And you will see the Son of Man sitting at the right hand of the Mighty One and coming on the clouds of heaven.”(BA)

63 The high priest tore his clothes.(BB) “Why do we need any more witnesses?” he asked. 64 “You have heard the blasphemy. What do you think?”

They all condemned him as worthy of death.(BC) 65 Then some began to spit at him; they blindfolded him, struck him with their fists, and said, “Prophesy!” And the guards took him and beat him.(BD)

Peter Disowns Jesus(BE)

66 While Peter was below in the courtyard,(BF) one of the servant girls of the high priest came by. 67 When she saw Peter warming himself,(BG) she looked closely at him.

“You also were with that Nazarene, Jesus,”(BH) she said.

68 But he denied it. “I don’t know or understand what you’re talking about,”(BI) he said, and went out into the entryway.[g]

69 When the servant girl saw him there, she said again to those standing around, “This fellow is one of them.” 70 Again he denied it.(BJ)

After a little while, those standing near said to Peter, “Surely you are one of them, for you are a Galilean.”(BK)

71 He began to call down curses, and he swore to them, “I don’t know this man you’re talking about.”(BL)

72 Immediately the rooster crowed the second time.[h] Then Peter remembered the word Jesus had spoken to him: “Before the rooster crows twice[i] you will disown me three times.”(BM) And he broke down and wept.

Footnotes

  1. Mark 14:5 Greek than three hundred denarii
  2. Mark 14:7 See Deut. 15:11.
  3. Mark 14:24 Some manuscripts the new
  4. Mark 14:27 Zech. 13:7
  5. Mark 14:30 Some early manuscripts do not have twice.
  6. Mark 14:36 Aramaic for father
  7. Mark 14:68 Some early manuscripts entryway and the rooster crowed
  8. Mark 14:72 Some early manuscripts do not have the second time.
  9. Mark 14:72 Some early manuscripts do not have twice.