Yesu Afufuka Kutoka Kwa Wafu

16 Sabato ilipomalizika, Mariamu Magdalena na Mariamu mama yake Yakobo na Salome walinunua manukato ili wakaupake mwili wa Yesu. Asubuhi na mapema, siku ya Jumapili, walikwenda kaburini jua likiwa linaanza kuchomoza. Njiani wakawa wanaulizana, “Ni nani atatuondolea lile jiwe kwenye mlango wa kaburi?” Lakini walipotazama, wakaona jiwe lile, ambalo lilikuwa kubwa sana, limekwisha ondolewa.

Walipoingia kaburini, walimwona kijana amekaa upande wa kulia akiwa amevaa vazi jeupe. Wakashtuka. Yule mtu akawaambia, “Msishtuke. Mnamtafuta Yesu Mnazareti, aliyesulubiwa. Amefufuka! Hayuko hapa! Tazameni mahali alipokuwa amelazwa.

Lakini nendeni mkawaambie wanafunzi wake, na Petro, kwamba anatangulia kwenda Galilaya na huko mtamwona, kama alivyowaam bia.” Wale wanawake wakiwa wanashangaa na kutetemeka kwa hofu, wakatoka pale kaburini mbio! Hawakumweleza mtu ye yote jambo lo lote kwa maana walikuwa wanaogopa.

Yesu Anamtokea Mariamu Magdalena

Baada ya Yesu kufufuka, alimtokea kwanza Mariamu Mag dalena, yule aliyemtoa pepo saba. 10 Mariamu akaenda akawaambia wale waliokuwa wakifuatana na Yesu. Wakati huo walikuwa bado wanalia na kuomboleza. 11 Lakini waliposikia kwamba Yesu yu hai na kwamba Mariamu alikuwa amemwona, hawakuamini.

Yesu Awatokea Wanafunzi Wawili

12 Baadaye Yesu aliwatokea kwa namna nyingine wanafunzi wawili walipokuwa wakienda shamba. 13 Nao pia walirudi wakawaam bia wenzao. Lakini pia hawakuamini.

Yesu Anawatokea Wale Wanafunzi Kumi Na Mmoja

14 Mwishowe, Yesu aliwatokea wale wanafunzi kumi na mmoja, wakiwa wanakula chakula. Akawakemea kwa kutokuamini kwao na kwa ugumu wa mioyo yao uliowafanya wakatae kuwasadiki wale waliomwona baada ya kufufuka.

15 Akawaambia, “Nendeni ulimwenguni kote, mkawahubirie watu wote Habari Njema. 16 Ye yote atakayeamini na kubatizwa ataoko lewa. Lakini ye yote ambaye atakataa kuamini, atahukumiwa.

17 “Na hizi ndizo ishara zitakazoandamana na wale wata kaoamini: Kwa kutumia jina langu watafukuza pepo; watasema kwa lugha mpya; 18 wataweza hata kuwakamata nyoka na kunywa sumu lakini wasidhurike; watawawekea wagonjwa mikono, nao watapona.”

Yesu Apaa Kwenda Mbinguni

19 Yesu alipokwisha kuwaambia maneno haya, alichukuliwa juu mbinguni, akaketi upande wa kulia wa Mungu.

Yesu Amefufuka Kutoka Mauti

(Mt 28:1-8; Lk 24:1-12; Yh 20:1-10)

16 Sabato ilipomalizika, Mariamu Magdalena, Maria mama yake Yakobo, na Salome wakanunua manukato yenye harufu nzuri ili kuyapaka kwenye mwili wa Yesu. Alfajiri na mapema Jumapili, mara tu baada ya jua kuchomoza, walienda kwenye kaburi la Yesu. Nao walikuwa wakiambiana wao kwa wao, ni nani atakayelivingirisha jiwe litoke katika mlango wa kaburi kwa ajili yetu?

Kisha wakatazama juu na wakaona kuwa jiwe lile kubwa lilikuwa limevingirishwa tayari litoke mlangoni mwa kaburi la Yesu. Walipoingia kaburini, wakamwona kijana mmoja ameketi upande wa kulia naye alikuwa amevaa vazi jeupe, nao wakastaajabu.

Naye akamwambia, “Usistaajabu. Unamtafuta Yesu wa Nazareti, aliyesulubiwa? Tazama amefufuka! Hayupo hapa. Angalieni mahali walipokuwa wameweka mwili wake. Hata hivyo nendeni na kuwaeleza wafuasi wake pamoja na Petro kwamba: ‘Ametangulia mbele yenu kuelekea Galilaya. Mtamkuta kule, kama alivyowaambia.’”

Kwa hiyo wale wanawake walitoka na kukimbia kutoka kaburini, kwa sababu hofu na mshangao ulikuwa umewajia. Nao hawakusema chochote kwa mtu yeyote kwani waliogopa.[a]

Baadhi ya Wafuasi Wamwona Yesu

(Mt 28:9-10; Yh 20:11-18; Lk 24:13-35)

Baada ya Yesu kufufuka alfajiri na mapema siku ya Jumapili, alimtokea kwanza Maria Magdalena, ambaye awali alifukuza mashetani saba kutoka kwake. 10 Baada ya Mariamu kumwona Yesu, alienda na kuwaeleza wanafunzi wake. Walikuwa wamehuzunishwa sana na walikuwa wakilia. 11 Lakini Mariamu aliwaambia kwamba Yesu yu hai. Aliwaambia ya kwamba yeye amemwona, lakini wao hawakumwamini.

12 Baada ya hayo, Yesu kwa namna tofauti akawatokea wanafunzi wake wawili walipokuwa wakitembea kuelekea mashambani. 13 Hawa kisha walirudi na wakawasimulia wengine wote, lakini nao hawakuwaamini.

Yesu Awatokea Wafuasi Wake

(Mt 28:16-20; Lk 24:36-49; Yh 20:19-23; Mdo 1:6-8)

14 Baadaye, Yesu aliwatokea wale mitume kumi na mmoja walipokuwa wakila. Naye akawakaripia kwa kutokuwa na imani. Walikuwa wakaidi na walikataa kuwaamini wale waliomwona Yesu baada ya kufufuka kwake.

15 Naye akawaambia, “Nendeni ulimwenguni pote, na mkahubiri Habari Njema kwa uumbaji wote. 16 Yeyote atakayeamini na kubatizwa ataokolewa, lakini yeyote asiyeamini atahukumiwa. 17 Na wale waaminio wataweza kufanya ishara hizi kama uthibitisho: watafukuza mashetani kwa jina langu; watasema kwa lugha mpya wasizojifunza bado; 18 watakamata nyoka kwa mikono yao; na ikiwa watakunywa sumu yoyote, haitawadhuru; wataweka mikono yao kwa wagonjwa, nao watapona.”

Yesu Arudi Mbinguni

(Lk 24:50-53; Mdo 1:9-11)

19 Hivyo baada ya Bwana Yesu kuzungumza nao, alichukuliwa mbinguni, kuketi katika mkono wa kuume wa Mungu. 20 Na mitume wakatoka na kwenda kuhubiri kila mahali, na Bwana alifanya kazi pamoja nao akithibitisha kuwa ujumbe wao ni wa kweli kwa ishara zilizofuatana na mahubiri yao.

Footnotes

  1. 16:8 Kitabu kinaishia hapa katika nakala mbili za zamani za Kiyunani zilizopatikana. Nakala chache nyingine za baadaye zina mwisho huu mfupi: “Lakini mara wakampa maagizo yote Petro na wale waliokuwa pamoja naye. Kisha Yesu mwenyewe akawatuma watoke na kwenda mashariki na magharibi wakiwa na ujumbe mtakatifu ambao kamwe hautabadilika; kwamba watu wataokolewa milele.”