Add parallel Print Page Options

Paulo na Barnaba Wakiwa Ikonia

14 Paulo na Barnaba walikwenda katika mji wa Ikonia. Kama walivyofanya Antiokia, waliingia katika sinagogi la Kiyahudi. Walizungumza na watu pale. Walizungumza kwa ushawishi sana kiasi kwamba Wayahudi na Wayunani wengi waliamini walichosema. Lakini Baadhi ya Wayahudi hawakuamini. Wayahudi hao walisema mambo yaliyowafanya wasio Wayahudi kukasirika na kuwa kinyume na waamini.

Hivyo Paulo na Barnaba walikaa Ikonia kwa muda mrefu, na walihubiri kwa ujasiri kwa ajili ya Bwana. Waliwahubiri watu kuhusu neema ya Mungu. Bwana alithibitisha kwamba kile walichosema ni kweli kwa ishara na maajabu yaliyofanyika kufanyika kupitia wao. Lakini baadhi ya watu katika mji wakakubaliana na Wayahudi ambao hawakuwaamini Paulo na Barnaba. Baadhi walikubaliana na mafundisho ya mitume. Hivyo mji uligawanyika.

Baadhi ya Wayahudi, viongozi wao na baadhi ya watu wasio wayahudi, walidhamiria kuwaumiza Paulo na Barnaba. Walitaka kuwaua kwa kuwapiga kwa mawe. Paulo na Barnaba walipotambua kuhusu hili, wakaondoka katika mji huo. Walikwenda Listra na Derbe, miji katika Likonia na maeneo yanayozunguka Likonia. Wakahubiri Habari Njema huko pia.

Paulo na Barnaba Wakiwa Listra na Derbe

Katika mji wa Listra kulikuwa mtu aliyekuwa na tatizo katika mguu wake. Alizaliwa akiwa mlemavu wa miguu na hakuwahi kutembea. Alikuwa amekaa akimsikiliza Paulo akizungumza. Paulo alipomwangalia kwa kumkazia macho alitambua kuwa mtu huyo alikuwa na imani kuwa Mungu angemponya. 10 Hivyo Paulo akapaza sauti na kumwambia, “Simama kwa miguu yako!” Mtu yule akaruka na kuanza kutembea.

11 Watu walipoona alichofanya Paulo, walipaza sauti kwa lugha yao wenyewe ya Kilikaonia. Walisema, “Miungu wamekuja kwetu katika maumbo ya kibinadamu!” 12 Watu wakaanza kumwita Barnaba “Zeusi”, na Paulo “Hermesi”, kwa sababu ndiye alikuwa mzungumzaji mkuu. 13 Hekalu la Zeusi lilikuwa karibu na mji. Kuhani wa hekalu hili alileta mafahari ya ng'ombe kadhaa na mashada ya maua[a] kwenye lango la mji. Kuhani na watu walitaka kuwatolea sadaka Paulo na Barnaba.

14 Lakini mitume, Barnaba na Paulo walipoelewa jambo ambalo watu walikuwa wanafanya, walirarua mavazi yao.[b] Kisha wakakimbia kuingia katikati ya watu na kuwaambia kwa kupaza sauti zao wakisema: 15 “Ndugu, kwa nini mnafanya hivi? Sisi si miungu. Ni wanadamu kama ninyi. Tulikuja kuwaambia Habari Njema. Tunawaambia mviache vitu hivi visivyo na thamani. Mgeukieni Mungu wa kweli aishiye, aliyeumba mbingu, nchi, bahari na vyote vilivyomo ndani yake.

16 Huko nyuma Mungu aliyaacha mataifa yote yatende yale waliyotaka. 17 Lakini daima Mungu alikuwepo na alitenda mambo mema yanayothibitisha kuwa yeye ni wa hakika na wa kweli. Huwapa mvua kutoka mbinguni na mavuno bora kwa wakati sahihi. Huwapa chakula tele na kuijaza mioyo yenu kwa furaha.”

18 Hata baada Paulo na Barnaba kusema hayo, hawakuweza kuwazuia watu kuwatolea sadaka za kuteketezwa.

19 Ndipo baadhi ya Wayahudi wakaja kutoka Antiokia na Ikonia na kuwashawishi watu ili wampinge Paulo. Hivyo wakamtupia mawe na kumburuza kumtoa nje ya mji. Wakidhani kuwa wamemwua. 20 Lakini wafuasi wa Yesu walipokusanyika kumzunguka, aliamka na kuingia mjini. Siku iliyofuata yeye na Barnaba waliondoka na kwenda katika mji wa Derbe.

Kurudi Antiokia ya Shamu

21 Walihubiri pia Habari Njema katika mji wa Derbe, na watu wengi wakawa wafuasi wa Yesu. Kisha Paulo na Barnaba walirudi katika miji ya Listra, Ikonia na Antiokia. 22 Katika miji hiyo waliwasaidia wafuasi kukua na kuwa na nguvu katika imani yao na waliwatia moyo kuendelea kumwamini Mungu. Waliwaambia, “Ni lazima tuteseke kwa mambo mengi katika safari yetu ya kwenda katika ufalme wa Mungu.” 23 Waliwachagua pia wazee katika kila kanisa na kuacha kula kwa muda ili kuwaombea. Wazee hawa walikuwa wanaume wanaomtumaini Bwana Yesu, hivyo Paulo na Barnaba wakamwomba Bwana awalinde.

24 Paulo na Barnaba walipita katikati ya eneo la Pisidia. Kisha walifika katika jimbo la Pamfilia. 25 Waliwahubiri watu ujumbe wa Mungu katika mji wa Perge, kisha wakateremka kwenda katika mji wa Attalia. 26 Na kutoka huko wakatweka tanga kwenda katika mji wa Antiokia ya Shamu. Huu ni mji ambako waamini waliwaweka katika uangalizi wa Mungu na kuwatuma kufanya kazi hii. Na sasa walikuwa wameimaliza.

27 Paulo na Barnaba walipofika, walilikusanya kanisa pamoja. Waliwaambia waamini yote ambayo Mungu aliwatumia kutenda. Walisema, “Mungu amefungua mlango kwa watu wasio Wayahudi kuamini!” 28 Na walikaa pale pamoja na wafuasi wa Bwana kwa muda mrefu.

Footnotes

  1. 14:13 mashada ya maua Wanyama waliotakiwa kutolewa dhabihu walivalishwa mashada haya kuzunguka shingo zao.
  2. 14:14 walirarua mavazi yao Hii ilionesha kuwa hawakufurahishwa na kitendo hicho.

In Iconium

14 At Iconium(A) Paul and Barnabas went as usual into the Jewish synagogue.(B) There they spoke so effectively that a great number(C) of Jews and Greeks believed. But the Jews who refused to believe stirred up the other Gentiles and poisoned their minds against the brothers.(D) So Paul and Barnabas spent considerable time there, speaking boldly(E) for the Lord, who confirmed the message of his grace by enabling them to perform signs and wonders.(F) The people of the city were divided; some sided with the Jews, others with the apostles.(G) There was a plot afoot among both Gentiles and Jews,(H) together with their leaders, to mistreat them and stone them.(I) But they found out about it and fled(J) to the Lycaonian cities of Lystra and Derbe and to the surrounding country, where they continued to preach(K) the gospel.(L)

In Lystra and Derbe

In Lystra there sat a man who was lame. He had been that way from birth(M) and had never walked. He listened to Paul as he was speaking. Paul looked directly at him, saw that he had faith to be healed(N) 10 and called out, “Stand up on your feet!”(O) At that, the man jumped up and began to walk.(P)

11 When the crowd saw what Paul had done, they shouted in the Lycaonian language, “The gods have come down to us in human form!”(Q) 12 Barnabas they called Zeus, and Paul they called Hermes because he was the chief speaker.(R) 13 The priest of Zeus, whose temple was just outside the city, brought bulls and wreaths to the city gates because he and the crowd wanted to offer sacrifices to them.

14 But when the apostles Barnabas and Paul heard of this, they tore their clothes(S) and rushed out into the crowd, shouting: 15 “Friends, why are you doing this? We too are only human,(T) like you. We are bringing you good news,(U) telling you to turn from these worthless things(V) to the living God,(W) who made the heavens and the earth(X) and the sea and everything in them.(Y) 16 In the past, he let(Z) all nations go their own way.(AA) 17 Yet he has not left himself without testimony:(AB) He has shown kindness by giving you rain from heaven and crops in their seasons;(AC) he provides you with plenty of food and fills your hearts with joy.”(AD) 18 Even with these words, they had difficulty keeping the crowd from sacrificing to them.

19 Then some Jews(AE) came from Antioch and Iconium(AF) and won the crowd over. They stoned Paul(AG) and dragged him outside the city, thinking he was dead. 20 But after the disciples(AH) had gathered around him, he got up and went back into the city. The next day he and Barnabas left for Derbe.

The Return to Antioch in Syria

21 They preached the gospel(AI) in that city and won a large number(AJ) of disciples. Then they returned to Lystra, Iconium(AK) and Antioch, 22 strengthening the disciples and encouraging them to remain true to the faith.(AL) “We must go through many hardships(AM) to enter the kingdom of God,” they said. 23 Paul and Barnabas appointed elders[a](AN) for them in each church and, with prayer and fasting,(AO) committed them to the Lord,(AP) in whom they had put their trust. 24 After going through Pisidia, they came into Pamphylia,(AQ) 25 and when they had preached the word in Perga, they went down to Attalia.

26 From Attalia they sailed back to Antioch,(AR) where they had been committed to the grace of God(AS) for the work they had now completed.(AT) 27 On arriving there, they gathered the church together and reported all that God had done through them(AU) and how he had opened a door(AV) of faith to the Gentiles. 28 And they stayed there a long time with the disciples.(AW)

Footnotes

  1. Acts 14:23 Or Barnabas ordained elders; or Barnabas had elders elected