28 Tulipofika salama nchi kavu, tuligundua kwamba tuko katika kisiwa kiitwacho Melita. Wenyeji wa kisiwa hicho walitufanyia ukarimu wa ajabu, wakawasha moto na kutukaribisha kwa maana mvua ilikuwa inanyesha na kulikuwa na baridi kali. Paulo alikuwa amekusanya kuni nyingi na alipokuwa akiziweka kwenye moto, aka toka humo nyoka mwenye sumu akikimbia ule moto akajisokotea kwe nye mkono wa Paulo. Wale wenyeji walipomwona yule nyoka ameji sokota kwenye mkono wa Paulo, wakaambiana, “Bila shaka mtu huyu ni muuaji, ijapokuwa ameokoka kufa maji baharini, haki haikumru husu aishi.” Lakini Paulo akamkung’utia yule nyoka ndani ya moto wala yeye hakupata madhara yo yote. Wakangojea wakitarajia kwamba atavimba au ataanguka ghafla na kufa. Lakini baada ya kungoja kwa muda mrefu na hawakuona dalili yo yote mbaya ikimto kea, wakabadili mawazo yao, wakasema yeye ni mungu.

Karibu na pwani ile, kulikuwa na shamba kubwa la gavana wa kisiwa kile aliyeitwa Publio. Huyu gavana alitukaribisha kwa ukarimu mkubwa, akatufanyia sherehe kwa muda wa siku tatu. Baba yake Publio alikuwa mgonjwa amelala, ana homa kali na kuhara damu. Paulo akaenda kumwona, akamwekea mikono akamwombea; naye akapona. Jambo hili lilipotokea, watu wote wa kisiwa kile wal iokuwa wagonjwa wakaja, nao wakaponywa. 10 Kwa hiyo wakatuletea zawadi nyingi, nasi tulipokuwa tukijiandaa kuondoka walitupatia kila kitu tulichohitaji kwa ajili ya safari.

Paulo Anawasili Rumi

11 Baada ya miezi mitatu tuliondoka kwa meli iliyokuwa ime toka Aleksandria ikawa imetia nanga katika kisiwa cha Melita mpaka majira ya baridi yaishe. Meli hiyo ilikuwa na picha ya miungu pacha Kasta na Poluksi. 12 Kituo chetu cha kwanza kili kuwa Sirakusa ambako tulikaa kwa siku tatu. 13 Kutoka huko tuka zunguka tukafika Regio; na baada ya siku moja, upepo mkali uka vuma kutoka kusini, na siku ya pili tukafika Puteoli. 14 Na hapa tuliwakuta waamini ambao walitukaribisha tukae nao kwa siku saba. Ndipo tukaendelea na safari mpaka tukafika Rumi. 15 Ndugu waamini wa Rumi walipopata habari zetu, walikuja mpaka soko la Apio na wengine wakaja mpaka mahali paitwapo ‘Mikahawa Mitatu’ kutulaki. Paulo alipowaona, alimshukuru Mungu akachangamka. 16 Tulipofika Rumi, Paulo aliruhusiwa kuishi peke yake akiwa na askari wa kumlinda.

Paulo Ahubiri Rumi

17 Baada ya siku tatu Paulo aliwaita pamoja viongozi wa Kiy ahudi wa Roma na walipofika Paulo akawaambia, “Ndugu zangu, ingawa sikufanya jambo lo lote kuwadhuru watu wetu au kinyume cha mila za baba zetu, hata hivyo nilikamatwa Yerusalemu nikakabid hiwa kwa utawala wa Kirumi. 18 Wao walipokwisha kunihoji wali taka kuniachilia huru kwa sababu hawakuona kosa lo lote nililoli fanya linalostahili adhabu ya kifo. 19 Lakini Wayahudi walipinga uamuzi huo, nililazimika kukata rufaa kwa Kaisari, ijapokuwa sikuwa na lalamiko lo lote juu ya taifa langu. 20 Hii ndio sababu nimeomba kuonana nanyi niwaeleze mambo haya. Kwa maana kusema kweli, nimevaa pingu hizi kwa sababu ya tumaini la Israeli.” 21 Wakamwambia, “Hatujapokea barua zo zote zinazoku husu wewe kutoka Yudea, wala hakuna ndugu ye yote aliyefika hapa ambaye ameleta ripoti mbaya kukuhusu. 22 Lakini tungependa kusi kia mawazo yako kwa sababu tunajua kwamba kila mahali watu wana zungumza mabaya kuhusu dhehebu hili.” 23 Basi wakapanga siku ya kumsikiliza, na ilipofika, wakaja watu wengi mahali alipokuwa anakaa Paulo. Akawaeleza kuhusu Ufalme wa Mungu tangu asubuhi hadi jioni, akijaribu kuwahakikishia juu ya Yesu akitumia Maan diko ya Musa na Manabii. 24 Baadhi yao wakakubali, wakaamini, lakini wengine wakakataa kuamini. 25 Kwa kuwa hawakukubaliana kati yao, wakaamua kuondoka, na walipokuwa tayari kuondoka, Paulo akawaambia, “Roho Mtakatifu alisema kweli alipowaambia baba zenu kupitia nabii Isaya: 26 ‘Nenda ukawaambie watu hawa, mtasikiliza na kusikiliza, lakini hamtaelewa. Mtatazama na kutazama lakini hamtatambua. 27 Kwa sababu mioyo ya watu hawa imepumbaa, masikio yao hayasikii na wamefunga macho yao. Kama si hivyo, wangeona kwa macho yao, wangesikia kwa masikio yao, wangeelewa kwa mioyo yao na kunigeukia; nami ningewaponya.’ 28 Kwa hiyo napenda mfahamu ya kuwa wokovu wa Mungu umepelekwa kwa watu wa mataifa; wao wata sikiliza.” 29 Baada ya Paulo kusema maneno haya Wayahudi wakaondoka wakibishana vikali wao kwa wao.] 30 Kwa muda wa miaka miwili Paulo aliishi katika nyumba ya kupangisha akiwakaribisha wote waliokuja kumwona.

Paulo Katika Kisiwa cha Malta

28 Tulipokuwa salama nchi kavu, tukatambua kuwa kisiwa kile kinaitwa Malta. Watu walioishi pale walikuwa wema sana kwetu. Mvua ilikuwa inanyesha na kulikuwa baridi sana, hivyo walitengeneza moto na kutukaribisha sote. Paulo alikusanya kuni nyingi kwa ajili ya moto. Alipokuwa akiweka kuni kwenye moto, nyoka mwenye sumu kali akajitokeza kwa sababu ya joto na kumuuma kwenye mkono. Wenyeji wa kisiwa kile walipomwona nyoka ananing'inia kwenye mkono wa Paulo, walisema, “Mtu huyu lazima ni mwuaji! Hakufa baharini, lakini Haki[a] hataki aishi.”

Lakini Paulo alimku'ngutia nyoka kwenye moto na hakudhurika. Watu wakadhani atavimba au ataanguka na kufa. Walisubiri na kumwangalia kwa muda mrefu, lakini hakuna kibaya kilichomtokea. Hivyo wakabadili mawazo yao. Wakasema, “Paulo ni mungu!”

Yalikuwepo mashamba kuzunguka eneo lile. Yaliyomilikiwa na ofisa wa juu sana wa Rumi katika kisiwa hicho aliyeitwa Pablio. Alitukaribisha nyumbani kwake na alikuwa mwema sana kwetu. Tulikaa nyumbani kwake kwa siku tatu. Baba yake Pablio alikuwa mgonjwa sana. Alikuwa na homa na alikuwa anaharisha damu, lakini Paulo alikwenda kwake na kumuombea. Aliweka mikono juu yake naye akapona. Baada ya hili kutokea, wagonjwa wengine wote kisiwani walikuja kwa Paulo, naye aliwaombea na wakaponywa pia.

10-11 Watu katika kisiwa hiki walituheshimu sana. Na baada ya kuwa pale kwa miezi mitatu, tukawa tayari kuondoka, walitupa kila kitu tulichohitaji kwa ajili ya safari yetu.

Paulo Aenda Rumi

Tulipanda meli iliyotoka Iskanderia iliyokaa katika kisiwa cha Malta wakati majira ya baridi. Mbele ya meli kulikuwa alama ya miungu pacha.[b] 12 Tulisimama katika mji wa Sirakuse. Tulikaa pale kwa siku tatu kisha tukaondoka. 13 Tulifika katika mji wa Regio. Siku iliyofuata upepo ulianza kuvuma kutokea Kusini-Magharibi, hivyo tuliweza kuondoka. Baada ya siku moja tukafika katika mji wa Puteoli. 14 Tuliwapata baadhi ya waamini pale, walituomba tukae nao kwa wiki moja. Mwishowe tulifika Rumi. 15 Ndugu na dada waliokaa Rumi walisikia habari zetu, walikuja kutupokea kwenye Soko la Apio[c] na kwenye Migahawa Mitatu.[d] Paulo alipowaona waamini hawa, alimshukuru Mungu na alifarijika.

Paulo Akiwa Rumi

16 Tulipofika Rumi, Paulo aliruhisiwa kuishi peke yake. Lakini askari alikaa pamoja naye kumlinda.

17 Siku tatu baadaye Paulo aliagiza baadhi ya Wayahudi muhimu waje kwake. Walipokusanyika, akasema, “Ndugu zangu, sijafanya lolote kinyume na watu wetu au kinyume na desturi za baba zetu. Lakini nilikamatwa Yerusalemu na kukabidhiwa kwa Warumi. 18 Waliniuliza maswali mengi, lakini hawakupata sababu yoyote kwa nini niuawe. Hivyo walitaka kuniachia huru. 19 Lakini Wayahudi kule hawakutaka hilo. Hivyo ilinibidi niombe kuja Rumi kuweka mashitaka yangu mbele ya Kaisari. Kwa kufanya hivi haimaanishi kuwa ninawashutumu watu wangu kwa kufanya chochote kibaya. 20 Ndiyo sababu nilitaka kuonana na kuzungumza nanyi. Nimefungwa kwa minyororo hii kwa sababu ninaamini katika tumaini la Israeli.”

21 Wayahudi walimjibu Paulo, “Hakuna barua tuliyoipokea kutoka Uyahudi kuhusu wewe. Hakuna ndugu yetu yeyote Myahudi aliyesafiri kutoka huko aliyeleta habari zako au kutwambia chochote kibaya juu yako. 22 Tunataka kusikia mawazo yako. Tunafahamu kuwa watu kila mahali wanapinga kundi hili jipya.”

23 Paulo na Wayahudi walichagua siku kwa ajili ya mkutano. Siku hiyo Wayahudi wengi walikutana na Paulo katika nyumba yake. Aliwaambia kwa siku nzima, akawafafanulia kuhusu ufalme wa Mungu. Alitumia Sheria ya Musa na maandishi ya manabii kuwashawishi kumwamini Yesu. 24 Baadhi ya Wayahudi waliamini alichosema, lakini wengine hawakuamini. 25 Walibishana wao wenyewe na wakaanza kuondoka. Lakini aliwaambia kitu kimoja zaidi: “Roho Mtakatifu aliwaambia ukweli baba zenu kupitia nabii Isaya, aliposema,

26 ‘Nenda kwa watu hawa na uwaambie:
Mtasikiliza na kusikiliza,
    lakini hamtaelewa.
Mtatazama na kutazama,
    lakini hakika hamtaona.
27 Watu hawa hawawezi kuelewa.
    Masikio yao yamezibwa.
    Na macho yao yamefumbwa.
Hivyo hawawezi kuona kwa macho yao,
    au kusikia kwa masikio yao;
    au kuelewa kwa akili zao;
    au kuelewa kwa akili zao.
Ikiwa wangeelewa, wangeweza kunirudia,
    na ningewaponya.’(A)

28 Ninataka ninyi Wayahudi mjue kuwa Mungu ameupeleka wokovu wake kwa watu wasio Wayahudi. Watasikia!” 29 [e]

30 Paulo alikaa katika nyumba yake mwenyewe aliyopanga kwa miaka miwili kamili. Aliwakaribisha watu wote waliokuja kumtembelea. 31 Aliwaambia kuhusu ufalme wa Mungu na kuwafundisha kuhusu Bwana Yesu Kristo. Alikuwa na ujasiri sana, na hakuna aliyejaribu kumzuia asizungumze.

Footnotes

  1. 28:4 Haki Wenyeji wa kisiwa kile waliamini kuwa kuna mungu mke aliyeitwa Haki ambaye angewaadhibu waovu.
  2. 28:10-11 miungu pacha Sanamu ya Kasto na Polu, miungu wa Kiyunani.
  3. 28:15 Soko la Apio Mji ulio kama maili 43 (kilomita 69) kutoka mji wa Rumi.
  4. 28:15 Migahawa Mitatu Mji ulio kama maili 30 (kilomita 48) kutoka mji wa Rumi.
  5. 28:29 Nakala zingine za baadaye za Matendo zimeongeza mstari wa 29: “Baada ya Paulo kusema hivi, Wayahudi walianza kuondoka, wakiwa bado wanabishana wao kwa wao.”

Paul Ashore on Malta

28 Once safely on shore, we(A) found out that the island(B) was called Malta. The islanders showed us unusual kindness. They built a fire and welcomed us all because it was raining and cold. Paul gathered a pile of brushwood and, as he put it on the fire, a viper, driven out by the heat, fastened itself on his hand. When the islanders saw the snake hanging from his hand,(C) they said to each other, “This man must be a murderer; for though he escaped from the sea, the goddess Justice has not allowed him to live.”(D) But Paul shook the snake off into the fire and suffered no ill effects.(E) The people expected him to swell up or suddenly fall dead; but after waiting a long time and seeing nothing unusual happen to him, they changed their minds and said he was a god.(F)

There was an estate nearby that belonged to Publius, the chief official of the island. He welcomed us to his home and showed us generous hospitality for three days. His father was sick in bed, suffering from fever and dysentery. Paul went in to see him and, after prayer,(G) placed his hands on him(H) and healed him.(I) When this had happened, the rest of the sick on the island came and were cured. 10 They honored us(J) in many ways; and when we were ready to sail, they furnished us with the supplies we needed.

Paul’s Arrival at Rome

11 After three months we put out to sea in a ship that had wintered in the island—it was an Alexandrian ship(K) with the figurehead of the twin gods Castor and Pollux. 12 We put in at Syracuse and stayed there three days. 13 From there we set sail and arrived at Rhegium. The next day the south wind came up, and on the following day we reached Puteoli. 14 There we found some brothers and sisters(L) who invited us to spend a week with them. And so we came to Rome. 15 The brothers and sisters(M) there had heard that we were coming, and they traveled as far as the Forum of Appius and the Three Taverns to meet us. At the sight of these people Paul thanked God and was encouraged. 16 When we got to Rome, Paul was allowed to live by himself, with a soldier to guard him.(N)

Paul Preaches at Rome Under Guard

17 Three days later he called together the local Jewish leaders.(O) When they had assembled, Paul said to them: “My brothers,(P) although I have done nothing against our people(Q) or against the customs of our ancestors,(R) I was arrested in Jerusalem and handed over to the Romans. 18 They examined me(S) and wanted to release me,(T) because I was not guilty of any crime deserving death.(U) 19 The Jews objected, so I was compelled to make an appeal to Caesar.(V) I certainly did not intend to bring any charge against my own people. 20 For this reason I have asked to see you and talk with you. It is because of the hope of Israel(W) that I am bound with this chain.”(X)

21 They replied, “We have not received any letters from Judea concerning you, and none of our people(Y) who have come from there has reported or said anything bad about you. 22 But we want to hear what your views are, for we know that people everywhere are talking against this sect.”(Z)

23 They arranged to meet Paul on a certain day, and came in even larger numbers to the place where he was staying. He witnessed to them from morning till evening, explaining about the kingdom of God,(AA) and from the Law of Moses and from the Prophets(AB) he tried to persuade them about Jesus.(AC) 24 Some were convinced by what he said, but others would not believe.(AD) 25 They disagreed among themselves and began to leave after Paul had made this final statement: “The Holy Spirit spoke the truth to your ancestors when he said(AE) through Isaiah the prophet:

26 “‘Go to this people and say,
“You will be ever hearing but never understanding;
    you will be ever seeing but never perceiving.”
27 For this people’s heart has become calloused;(AF)
    they hardly hear with their ears,
    and they have closed their eyes.
Otherwise they might see with their eyes,
    hear with their ears,
    understand with their hearts
and turn, and I would heal them.’[a](AG)

28 “Therefore I want you to know that God’s salvation(AH) has been sent to the Gentiles,(AI) and they will listen!” [29] [b]

30 For two whole years Paul stayed there in his own rented house and welcomed all who came to see him. 31 He proclaimed the kingdom of God(AJ) and taught about the Lord Jesus Christ—with all boldness(AK) and without hindrance!

Footnotes

  1. Acts 28:27 Isaiah 6:9,10 (see Septuagint)
  2. Acts 28:29 Some manuscripts include here After he said this, the Jews left, arguing vigorously among themselves.