Uchaguzi Wa Wahudumu

Siku hizo, wakati idadi ya waamini ilipokuwa ikiongezeka sana palitokea manung’uniko. Wayahudi walioongea lugha ya Kigi riki walilalamika kuwa wakati wa kugawa chakula, wajane walioon gea Kiebrania walipendelewa na wajane wao walibaguliwa. Wale mitume kumi na wawili waliitisha kikao cha wanafunzi wote, wakasema, “Si sawa sisi tuache kazi ya kuhubiri neno la Mungu tuanze kugawa chakula. Kwa hiyo ndugu, chagueni watu saba mion goni mwenu; watu wenye sifa njema, waliojawa na Roho Mtakatifu na hekima, ili tuwakabidhi kazi hii. Na sisi tutatumia wakati wetu kwa kuomba na kufundisha neno la Bwana.”

Uamuzi huu ukawaridhisha wote nao wakawachagua Stefano, mtu aliyejawa na imani na Roho Mtakatifu; na Filipo, Prokoro, Nika nori, na Timoni, Parmena na Nikolao mwongofu wa kutoka Antiokia. Wakawaleta watu hawa mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono juu yao.

Na neno la Mungu likazidi kuenea; idadi ya wanafunzi ika zidi kuongezeka sana katika Yerusalemu, na hata makuhani wengi wakamwamini Yesu.

Stefano Akamatwa

Na Stefano akiwa amejawa na neema na nguvu za Mungu alifa nya maajabu makubwa na ishara kati ya watu.

Lakini baadhi ya watu wa sinagogi lililoitwa la ‘Watu Huru,’ na wengine kutoka masinagogi ya Kirene na Aleksandria, pamoja na baadhi kutoka Kilikia na Asia, wakajaribu kubishana na Stefano. 10 Lakini hawakuweza kushindana naye kwa sababu ya hekima yake na Roho aliyemwezesha kusema.

11 Ndipo wakawashawishi watu fulani ambao walisema, “Tulim sikia akisema maneno ya kufuru juu ya Musa na Mungu.”

Stefano Afikishwa Mbele Ya Baraza

12 Wakawachochea watu, wazee na waandishi wa sheria nao wakamkamata Stefano wakamfikisha mbele ya baraza. 13 Wakaweka mashahidi wa uongo ambao walisema, “Mtu huyu siku zote anasema maneno ya kashfa juu ya Hekalu hili takatifu na juu ya sheria za Musa. 14 Kwa maana tumemsikia akisema kwamba eti huyu Yesu wa Nazareti ataharibu hili Hekalu takatifu na atabadilisha mila zote tulizopewa na Musa.” 15 Watu wote waliokuwa katika baraza hilo walimtazama Stefano kwa makini wakaona uso wake unang’aa kama uso wa malaika! Hotuba Ya Stefano

The Choosing of the Seven

In those days when the number of disciples was increasing,(A) the Hellenistic Jews[a](B) among them complained against the Hebraic Jews because their widows(C) were being overlooked in the daily distribution of food.(D) So the Twelve gathered all the disciples(E) together and said, “It would not be right for us to neglect the ministry of the word of God(F) in order to wait on tables. Brothers and sisters,(G) choose seven men from among you who are known to be full of the Spirit(H) and wisdom. We will turn this responsibility over to them(I) and will give our attention to prayer(J) and the ministry of the word.”

This proposal pleased the whole group. They chose Stephen,(K) a man full of faith and of the Holy Spirit;(L) also Philip,(M) Procorus, Nicanor, Timon, Parmenas, and Nicolas from Antioch, a convert to Judaism. They presented these men to the apostles, who prayed(N) and laid their hands on them.(O)

So the word of God spread.(P) The number of disciples in Jerusalem increased rapidly,(Q) and a large number of priests became obedient to the faith.

Stephen Seized

Now Stephen, a man full of God’s grace and power, performed great wonders and signs(R) among the people. Opposition arose, however, from members of the Synagogue of the Freedmen (as it was called)—Jews of Cyrene(S) and Alexandria as well as the provinces of Cilicia(T) and Asia(U)—who began to argue with Stephen. 10 But they could not stand up against the wisdom the Spirit gave him as he spoke.(V)

11 Then they secretly(W) persuaded some men to say, “We have heard Stephen speak blasphemous words against Moses and against God.”(X)

12 So they stirred up the people and the elders and the teachers of the law. They seized Stephen and brought him before the Sanhedrin.(Y) 13 They produced false witnesses,(Z) who testified, “This fellow never stops speaking against this holy place(AA) and against the law. 14 For we have heard him say that this Jesus of Nazareth will destroy this place(AB) and change the customs Moses handed down to us.”(AC)

15 All who were sitting in the Sanhedrin(AD) looked intently at Stephen, and they saw that his face was like the face of an angel.

Footnotes

  1. Acts 6:1 That is, Jews who had adopted the Greek language and culture