Wimbo Wa Ushindi

19 Baada ya haya nikasikia sauti kama sauti kuu ya umati mkubwa wa watu mbinguni ikisema kwa nguvu, “Haleluya! Wokovu na utukufu na uweza ni wa Mungu wetu. Maana hukumu zake ni za kweli na haki, amemhukumu yule kahaba mkuu aliyeuharibu ulimwengu kwa uasherati wake. Mungu amelipiza kisasi kwa ajili ya damu ya watumishi wake.” Kwa mara nyingine wakasema kwa nguvu, “Hale luya! Moshi wake huyo kahaba unapanda juu milele na milele.” Wale wazee ishirini na wanne pamoja na wale viumbe wanne wenye uhai walianguka kifudifudi wakamwabudu Mungu aliyekuwa ameketi katika kiti cha enzi. Wakasema kwa sauti kuu, “Amina! Hale luya!”

Na sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi ikisema, “Msi funi Mungu wetu ninyi watumishi wake wote, nyote mnaomcha, wadogo kwa wakubwa.”

Kisha nikasikia sauti kama sauti ya umati mkubwa wa watu, kama sauti ya maporomoko ya maji mengi na kama ngurumo kuu ya radi kubwa ikisema, “Haleluya! Kwa maana Bwana Mungu wetu Mwe nyezi anatawala. Tufurahi na kushangilia na kumtukuza maana harusi ya Mwana-Kondoo imefika na bibi harusi wake amejitayar isha. Alipewa kitani safi nyeupe inayong’aa ili avae.” Hiyo kitani safi ni matendo ya haki ya watakatifu.

Na malaika akaniambia, “Andika haya: ‘Wamebarikiwa wal ioalikwa kwenye karamu ya harusi ya Mwana-Kondoo.”’ Na akaniambia, “Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu.”

10 Ndipo nikaanguka kifudifudi miguuni pake kumwabudu, lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi pia ni mtumishi pamoja na wewe na ndugu zako wanaoshikilia ushuhuda wao kwa Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ushuhuda wa Yesu ndio kiini cha unabii.”

Aliyepanda Farasi Mweupe

11 Kisha nikaona mbingu imefunguka na mbele yangu nikaona farasi mweupe! Aliyeketi juu ya huyo farasi aliitwa Mwaminifu na Kweli, naye huhukumu na kupigana vita kwa ajili ya haki. 12 Macho yake ni kama miali ya moto na juu ya kichwa chake kuna vilemba vingi; na ameandikwa jina ambalo hakuna mwingine anayeli jua isipokuwa yeye mwenyewe. 13 Amevaa vazi lililochovywa katika damu na jina analoitwa ni “Neno la Mungu”. 14 Na majeshi ya mbinguni yaliyovaa kitani safi nyeupe walimfuata wakiwa wamepanda farasi weupe.

15 Kinywani mwake mlitoka upanga mkali wa kuyapiga mataifa. Atawatawala kwa fimbo ya chuma na kukamua divai katika mtambo wa kutengenezea divai ya ghadhabu ya Mungu Mwenyezi. 16 Kwenye vazi lake na paja lake liliandikwa jina hili: “Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana.”

Bwana wa mabwana.”

17 Kisha nikamwona malaika amesimama ndani ya jua, akaita ndege wote warukao angani kwa sauti kuu, “Njooni, kusanyikeni kwa ajili ya karamu kubwa ya Mungu. 18 Njooni mle nyama ya wafalme na nyama ya majemadari, na nyama ya watu hodari; nyama ya farasi na wapanda farasi, nyama ya wanadamu wote, wakubwa kwa wadogo, watumwa na watu huru.”

19 Na nikamwona yule mnyama na wafalme wa duniani pamoja na majeshi yao wakikusanyika kumpiga vita yeye aketiye juu ya yule farasi pamoja na jeshi lake. 20 Yule mnyama akatekwa pamoja na yule nabii wa uongo, aliyefanya ishara za uongo, kwa niaba yake, akawadanganya wale waliopokea alama ya huyo mnyama na kuiabudu sanamu yake. Hawa wawili walitupwa wangali hai katika ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. 21 Waliobakia waliuawa kwa upanga wa yule aketiye juu ya farasi, kwa ule upanga utokao kinywani mwake; na ndege wote wakala nyama yao mpaka wakakinai.