Watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, kwa maana kufanya hivyo ni vizuri. “Waheshimu baba yako na mama yako,” hii ndio amri ya kwanza yenye ahadi, “upate baraka na uishi siku nyingi duniani.” Akina baba, msiwachokoze watoto wenu, bali waleeni kwa nidhamu na mafundisho ya Bwana. Watumwa Na Mabwana

Watumwa, watiini hao walio mabwana zenu hapa duniani, kwa heshima na kwa kutetemeka na kwa moyo mmoja, kama vile mnamtii Kristo. Watiini, sio tu wakati wakiwaona ili mpate sifa, bali mtumike kama watumishi wa Kristo, mkifanya mapenzi ya Mungu kwa moyo. Toeni huduma yenu kwa moyo wote, kama vile mnamtumikia Bwana na sio watu. Mkumbuke kuwa Bwana atampa kila mmoja tuzo kutegemeana na wema aliotenda, kama yeye ni mtumwa au ni mtu huru. Nanyi mabwana watendeeni watumwa wenu kwa jinsi hiyo hiyo. Msiwatishe, kwa kuwa mnajua ya kwamba yeye aliye Bwana wenu na wao yuko mbinguni, naye hana upendeleo.

10 Hatimaye, muwe imara katika Bwana na katika nguvu zake kuu. 11 Vaeni silaha zote za Mungu ili mpate kusimama na kupin gana na hila zote za shetani. 12 Kwa maana hatupambani na bina damu, bali tunapambana na tawala na mamlaka na nguvu za ulimwengu huu wa giza na majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. 13 Kwa hiyo, vaeni silaha zote za Mungu ili mpate kusimama imara siku ya uovu itakapokuja; na mkishafanya yote, mtakuwa bado mme simama. 14 Kwa hiyo simameni imara mkisha jifunga na kweli kama mkanda kiunoni na haki kama kinga ya kifuani; 15 na kuvaa Injili ya amani kama viatu miguuni, ili muweze kusimama barabara. 16 Zaidi ya haya yote, jivikeni imani kama ngao ambayo itawawe zesha kuzuia mishale yenye miale ya moto kutoka kwa yule mwovu. 17 Vaeni wokovu kama kofia ya vita vichwani na chukueni upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu. 18 Ombeni wakati wote katika Roho, katika sala zote na maombi. Kwa hiyo muwe macho na siku zote endeleeni kuwaombea watu wote wa Mungu. 19 Niombeeni mimi pia, ili kila ninapozungumza, nipewe maneno ya kusema, niweze kutangaza siri ya Injili pasipo woga. 20 Mimi ni balozi kifun goni kwa ajili ya Injili hii. Kwa hiyo niombeeni niihubiri Injili kwa ujasiri kama inipasavyo. 21 Ndugu mpendwa Tikiko, ambaye ni mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawaelezeni kila kitu ili mjue habari zangu na mfahamu ninachofanya. 22 Ninamtuma kwenu kwa kusudi hili, mpate habari zetu naye awafariji. 23 Nawatakia ndugu wote amani na upendo pamoja na imani kutoka kwa Mungu Baba na Bwana wetu Yesu Kristo.

Watoto na Wazazi Wao

Watoto, watiini wazazi wenu katika namna ambayo Bwana anataka, kwa sababu hili ni jambo sahihi kutenda. Amri husema, “Waheshimu baba yako na mama yako.”(A) Hii ndiyo amri ya kwanza iliyo na ahadi pamoja nayo. Na hii ndiyo ahadi: “Ndipo utakapofanikiwa, na utakuwa na maisha marefu duniani.”(B)

Wababa, msiwakasirishe watoto wenu, lakini waleeni kwa mafunzo na mausia mliyopokea kutoka kwa Bwana.

Watumwa na Bwana

Watumwa, watiini bwana zenu hapa duniani kwa hofu na heshima. Na fanyeni hivi kwa moyo ulio wa kweli, kama mnavyomtii Kristo. Mfanye hivi siyo tu kwa kuwafurahisha bwana zenu wakati wanapowaona, bali wakati wote. Kwa vile ninyi hakika ni watumwa wa Kristo, mfanye kwa mioyo yenu yale Mungu anayotaka. Fanyeni kazi zenu, na mfurahie kuzifanya. Fanyeni kana kwamba mnamtumikia Bwana, siyo tu bwana wa duniani. Kumbukeni kwamba Bwana atampa kila mmoja zawadi kwa kufanya vema. Kila mmoja, mtumwa au aliye huru, atapata zawadi kwa mambo mema aliyotenda.

Mabwana, kwa jinsi hiyo hiyo, muwe wema kwa watumwa wenu. Msiseme mambo ya kuwatisha. Mnajua kuwa yeye aliye Bwana wenu na Bwana wao yuko mbinguni, na humchukulia kila mmoja sawa.

Vaeni Silaha Zote za Mungu

10 Hapa lipo neno moja la mwisho la ushauri: Mtegemeeni Bwana kwa ajili ya nguvu zenu. Wekeni matumaini yenu katika nguvu zake kuu. 11 Vaeni silaha zote za Mungu ili mweze kupigana dhidi ya hila za Shetani. 12 Mapigano yetu si juu ya watu duniani. Tunapigana dhidi ya watawala, mamlaka na nguvu za giza za ulimwengu huu. Tunapigana dhidi ya nguvu za uovu katika ulimwengu wa roho. 13 Ndiyo sababu mnahitaji silaha zote za Mungu. Ili siku ya uovu, mweze kusimama imara. Na mtakapomaliza mapigano yote, mtaendelea kusimama.

14 Hivyo simameni imara mkiwa mmefungwa mkanda wa kweli viunoni mwenu, na katika vifua vyenu mkiwa mmevaa kinga ya maisha ya haki. 15 Miguuni mwenu vaeni Habari Njema za amani ili ziwasaidie msimame imara. 16 Pia itumieni ngao ya imani ambayo itatumika kuizuia mishale inayowaka moto inayotoka kwa yule Mwovu. 17 Upokeeni wokovu wa Mungu kama chapeo yenu. Na chukueni upanga wa Roho, yaani mafundisho ya Mungu. 18 Ombeni katika Roho kila wakati. Ombeni maombi ya aina zote, na ombeni kila mnachohitaji. Ili mfanye hivi ni lazima muwe tayari. Msikate tamaa. Waombeeni watu wa Mungu daima.

19 Pia ombeni kwa ajili yangu ili ninapoongea, Mungu anipe maneno ili niweze kusema siri ya kweli juu ya Habari Njema bila woga. 20 Ninayo kazi ya kuhubiri Habari Njema, na hicho ndicho ninachofanya sasa humu gerezani. Niombeeni ili ninapowahubiri watu Habari Njema, nihubiri kwa ujasiri kama inavyonipasa kuhubiri.

Salamu za Mwisho

21 Namtuma kwenu Tikiko, ndugu yetu mpendwa na msaidizi mwaminifu katika kazi ya Bwana. Atawaeleza kila kitu kinachonipata. Kisha mtaelewa jinsi nilivyo na ninachofanya. 22 Ndiyo sababu namtuma yeye ili awajulishe hali zetu na tuwatie moyo.

23 Namwomba Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo awape amani, upendo na imani ndugu zangu wote mlio huko. 24 Naomba neema ya Mungu iwe pamoja nanyi nyote mnaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa pendo lisilo na mwisho.

Children, obey your parents in the Lord, for this is right.(A) “Honor your father and mother”—which is the first commandment with a promise— “so that it may go well with you and that you may enjoy long life on the earth.”[a](B)

Fathers,[b] do not exasperate your children;(C) instead, bring them up in the training and instruction of the Lord.(D)

Slaves, obey your earthly masters with respect(E) and fear, and with sincerity of heart,(F) just as you would obey Christ.(G) Obey them not only to win their favor when their eye is on you, but as slaves of Christ,(H) doing the will of God from your heart. Serve wholeheartedly, as if you were serving the Lord, not people,(I) because you know that the Lord will reward each one for whatever good they do,(J) whether they are slave or free.

And masters, treat your slaves in the same way. Do not threaten them, since you know that he who is both their Master and yours(K) is in heaven, and there is no favoritism(L) with him.

The Armor of God

10 Finally, be strong in the Lord(M) and in his mighty power.(N) 11 Put on the full armor of God,(O) so that you can take your stand against the devil’s schemes. 12 For our struggle is not against flesh and blood,(P) but against the rulers, against the authorities,(Q) against the powers(R) of this dark world and against the spiritual forces of evil in the heavenly realms.(S) 13 Therefore put on the full armor of God,(T) so that when the day of evil comes, you may be able to stand your ground, and after you have done everything, to stand. 14 Stand firm then, with the belt of truth buckled around your waist,(U) with the breastplate of righteousness in place,(V) 15 and with your feet fitted with the readiness that comes from the gospel of peace.(W) 16 In addition to all this, take up the shield of faith,(X) with which you can extinguish all the flaming arrows of the evil one.(Y) 17 Take the helmet of salvation(Z) and the sword of the Spirit,(AA) which is the word of God.(AB)

18 And pray in the Spirit(AC) on all occasions(AD) with all kinds of prayers and requests.(AE) With this in mind, be alert and always keep on praying(AF) for all the Lord’s people. 19 Pray also for me,(AG) that whenever I speak, words may be given me so that I will fearlessly(AH) make known the mystery(AI) of the gospel, 20 for which I am an ambassador(AJ) in chains.(AK) Pray that I may declare it fearlessly, as I should.

Final Greetings

21 Tychicus,(AL) the dear brother and faithful servant in the Lord, will tell you everything, so that you also may know how I am and what I am doing. 22 I am sending him to you for this very purpose, that you may know how we are,(AM) and that he may encourage you.(AN)

23 Peace(AO) to the brothers and sisters,[c] and love with faith from God the Father and the Lord Jesus Christ. 24 Grace to all who love our Lord Jesus Christ with an undying love.[d]

Footnotes

  1. Ephesians 6:3 Deut. 5:16
  2. Ephesians 6:4 Or Parents
  3. Ephesians 6:23 The Greek word for brothers and sisters (adelphoi) refers here to believers, both men and women, as part of God’s family.
  4. Ephesians 6:24 Or Grace and immortality to all who love our Lord Jesus Christ.