Mfano Wa Abrahamu

Tusemeje basi kuhusu baba yetu Abrahamu? Yeye alijifunza nini? Ikiwa Abrahamu alihesabiwa haki kwa matendo, basi anacho kitu cha kujivunia, lakini si mbele za Mungu. Maandiko yanase maje? “Abrahamu alimwamini Mungu na kwa ajili ya imani yake aka hesabiwa haki.”

Mtu akifanya kazi, mshahara wake hauhesabiwi kuwa ni zawadi bali ni haki yake. Lakini kwa mtu ambaye hakufanya kazi ila amemtegemea Mungu anayewahesabia haki waovu, imani yake inahesabiwa kuwa haki. Daudi pia ana maana hiyo hiyo anapoongea juu ya baraka apatazo mtu ambaye Mungu amemhesabia haki pasipo kutenda lo lote: “Wamebarikiwa wale ambao makosa yao yamesame hewa, ambao dhambi zao zimefunikwa. Amebarikiwa mtu ambaye Bwana hamhesabii dhambi zake.”

Haki Kabla Ya Tohara

Je, baraka hii anayosema Daudi ni ya wale waliotahiriwa tu au pia ni ya wale wasiotahiriwa? Tunasema kwamba imani ya Abra hamu ilihesabiwa kama haki. 10 Je, hii ilitokea wakati gani? Je, ilikuwa ni kabla au baada ya kutahiriwa kwake? Haikuwa baada, ila kabla hajatahiriwa. 11 Na alipewa tohara kama alama na mhuri wa haki aliyoipokea kwa imani hata kabla ya kutahiriwa. Shabaha ya Mungu ilikuwa kwamba Abrahamu awe baba ya wote wenye imani ambao bado hawajatahiriwa ili wao pia wahesabiwe haki. 12 Pia yeye ni baba wa wale waliokwisha kutahiriwa ambao si kwamba wametahiriwa tu, bali pia wanafuata mfano wa imani aliyokuwanayo baba yetu

Haki Haipatikani Kwa Sheria

13 Ahadi ambayo Mungu alimpa Abrahamu na kizazi chake, kwamba ataurithi ulimwengu, haikutolewa kwa kuwa Abrahamu alitii sheria lakini ni kwa sababu alikuwa na imani, na Mungu akaihesabu imani yake kuwa ni haki. 14 Ikiwa wafuatao sheria tu ndio wata kaopewa urithi ulioahidiwa na Mungu, basi imani si kitu na ahadi hiyo haina thamani. 15 Kwa maana sheria huleta ghadhabu ya Mungu na ambapo hakuna sheria basi hakuna makosa.

16 Ndio maana ahadi hiyo ilitolewa kwa msingi wa imani, ili ipatikane bure kwa neema na ithibitishwe kwa vizazi vyote vya Abrahamu, si wale tu walio na sheria, bali pia na wale wenye imani ya Abrahamu. Kwa maana yeye ni baba yetu sote. 17 Kama ilivyoandikwa: “Nimekufanya wewe kuwa baba wa mataifa mengi.” Yeye ni baba yetu mbele za Mungu aliyemwamini. Mungu ambaye ana wapa wafu uhai na ambaye huamuru vitu ambavyo havipo viwepo.

Mfano Wa Imani Ya Abrahamu

18 Ijapokuwa ilionekana kama matumaini ya Ibrahimu yalikuwa ya bure, yeye alimtumaini na kumwamini Mungu na kwa kufanya hivyo akawa baba wa mataifa mengi, kama alivyokuwa ameahidiwa kwamba, “Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.” 19 Ijapokuwa mwili wake hau kuwa tena na uwezo wa kuzaa, alikuwa na umri upatao miaka mia moja na Sara alishapita umri wa kuzaa, imani yake haikufifia. 20 Abrahamu hakuacha kuamini wala hakuwa na mashaka juu ya ahadi ya Mungu. Imani yake ilimtia nguvu, akamtukuza Mungu, 21 akiwa na hakika kabisa kwamba Mungu alikuwa na uwezo wa kutimiza ali loahidi. 22 Ndio sababu imani yake, “ilihesabiwa kwake kuwa ni haki.” 23 Maneno haya, “ilihesabiwa kwake kuwa ni haki,” hay akuandikwa kwa ajili yake peke yake 24 bali kwetu pia. Tutahe sabiwa haki sisi tunaomwamini Mungu aliyemfufua Bwana wetu Yesu kutoka kwa wafu. 25 Yesu aliuawa kwa ajili ya dhambi zetu na kufufuliwa ili tuhesabiwe haki.

Mfano wa Ibrahimu

Basi tuseme nini kuhusu Ibrahimu,[a] baba wa watu wetu? Ikiwa Ibrahimu alifanywa kuwa mwenye haki kutokana na matendo yake, hicho ni kitu cha kujivunia! Lakini kama Mungu aonavyo, hakuwa na sababu ya kujivuna. Hili ni wazi kama Maandiko yanavyosema, “Ibrahimu alimwamini Mungu, na kwa sababu ya kuamini kwake, Mungu alimhesabu kuwa mwenye haki.”[b]

Watu wanapofanya kazi, mshahara wao hautolewi kama zawadi. Ni kitu wanachopata kutokana na kazi waliyofanya. Lakini watu hawawezi kufanya kazi yoyote itakayowafanya wahesabiwe kuwa wenye haki mbele za Mungu. Hivyo ni lazima wamtumaini Yeye. Kisha huikubali imani yao na kuwahesabia haki. Yeye ndiye anayewahesabia haki hata waovu. Daudi alisema mambo hayo hayo alipozungumzia baraka wanazopata watu pale Mungu anapowahesabia haki pasipo kuangalia matendo yao:

“Ni heri kwa watu
    wanaposamehewa kutokana na mabaya waliyotenda,
    dhambi zao zinapofutwa!
Ni heri kwa watu,
    Bwana anapozifuta dhambi zao kutoka katika kumbukumbu yake!”(A)

Je, baraka hii ni kwa ajili ya waliotahiriwa tu? Au pia ni kwa ajili ya wale wasiotahiriwa? Tumekwisha sema ya kwamba Ibrahimu alikubaliwa kuwa ni mwenye haki mbele za Mungu kutokana na imani yake. 10 Sasa katika mazingira gani hili lilitokea? Je, Mungu alimkubali Ibrahimu na kumhesabia haki kabla au baada ya kutahiriwa? Mungu alimkubali kabla ya kutahiriwa kwake. 11 Ibrahimu alitahiriwa baadaye ili kuonesha kuwa Mungu amemkubali kuwa mwenye haki. Tohara yake ilikuwa uthibitisho kwamba Mungu alimhesabia haki kwa njia ya imani hata kabla ya kutahiriwa. Hivyo Ibrahimu ni baba wa wote wanaoamini lakini hawajatahiriwa. Kama Ibrahimu, wao pia wamekubaliwa na Mungu kuwa wenye haki kwa sababu ya imani yao tu. 12 Pia Ibrahimu ni baba wa waliotahiriwa, lakini si kwa sababu ya kutahiriwa kwao. Ni baba yao kwa sababu wao nao wamemwamini Mungu vile vile kama Ibrahimu alivyofanya kabla hajatahiriwa.

Ahadi ya Mungu Hupokelewa kwa Imani

13 Mungu aliweka ahadi kwa Ibrahimu na wazaliwa wake ya kuwapa ulimwengu wote. Lakini kwa nini Mungu aliweka ahadi hii? Haikuwa kwa sababu Ibrahimu aliifuata sheria. Ni kwa sababu aliiweka imani yake katika Mungu na akakubaliwa kuwa mwenye haki. 14 Watu wa Mungu watarithi yote ambayo Mungu alimwahidi Ibrahimu, lakini si kwa sababu wanaifuata sheria. Ikiwa ni lazima tuitii sheria ili tupate kile alichoahidi Mungu, badi imani ya Ibrahimu haina maana yoyote na ahadi ya Mungu haina manufaa. 15 Ninasema hivi kwa sababu sheria ndiyo huleta hasira ya Mungu kwa wale wasioitii. Lakini ikiwa sheria haipo, basi hakuna hatia ya kutoitii.

16 Hivyo watu hupokea ahadi ya Mungu kwa imani. Hili hutokea ili ahadi hiyo iwe kipawa cha bure. Na ikiwa ahadi ni kipawa cha bure, basi watu wote wa Ibrahimu watapata ahadi hiyo. Ahadi hii si tu kwa ajili ya wale wanaoishi chini ya Sheria ya Musa. Bali ni kwa ajili ya wote wanaoishi kwa kuweka imani yao kwa Mungu kama Ibrahimu alivyofanya. Ni baba yetu sote. 17 Kama Maandiko yanavyosema, “Nimekufanya uwe baba wa mataifa mengi.”(B) Ibrahimu aliposikia ahadi hii, aliiweka imani yake kwa Mungu. Mungu ndiye awapaye uhai waliokufa na kwa amri yake huumba kisichokuwepo.

18 Halikuwepo tumaini kwamba Ibrahimu angepata watoto, lakini alimwamini Mungu na akaendelea kutumaini. Na ndiyo sababu akafanyika kuwa baba wa mataifa mengi. Kama Mungu alivyomwambia kuwa, “Utakuwa na wazaliwa wengi.”(C) 19 Ibrahimu alikuwa na umri uliokaribia miaka 100, hivyo alikuwa amevuka umri wa kupata watoto. Pia, Sara hakuweza kuwa na watoto. Ibrahimu alilijua hili vizuri, lakini imani yake kwa Mungu haikudhoofika. 20 Hakutilia shaka kuwa Mungu angetenda kile alichoahidi. Hakuacha kuamini. Kwa hakika, aliendelea kuimarika katika imani yake. Alitukuza Mungu 21 na alikuwa na uhakika kuwa Mungu anaweza kutenda alichoahidi. 22 Ndiyo sababu “Mungu alimkubali kuwa ni mwenye haki”. 23 Maneno haya, “alikubaliwa”, yaliandikwa siyo tu kwa ajili ya Ibrahimu. 24 Pia yaliandikwa kwa ajili yetu. Mungu atatukubali sisi pia kwa sababu tunaamini. Tunamwamini yule aliyemfufua Yesu Bwana wetu kutoka kwa wafu. 25 Yesu alitolewa afe kwa ajili ya dhambi zetu, na akafufuliwa kutoka kifo ili Mungu atuhesabie haki.

Footnotes

  1. 4:1 Basi tuseme nini kuhusu Ibrahimu Au, “Tuseme tumeona nini [katika Sheria] kuhusu Ibrahimu?”
  2. 4:3 Mwa 15:6. Pia katika mstari wa 9 na 22.