Onyo Kwa Matajiri

Sasa sikilizeni, ninyi matajiri: Lieni na kuomboleza kwa ajili ya huzuni inayowajia. Utajiri wenu umeoza na mavazi yenu yameliwa na nondo. Dhahabu yenu na fedha yenu vimeingia kutu na kutu yake itakuwa ushahidi dhidi yenu na itakula miili yenu kama moto. Mmejilimbikizia utajiri kwa siku za mwisho. Angalieni ule ujira mliowadhulumu vibarua waliovuna mashamba yenu unawalilia; na vilio vya wavunaji hao vimeyafikia masikio ya Bwana wa majeshi. Mmeishi duniani maisha ya anasa na kujistarehesha. Mmejinenepesha tayari kwa siku ya kuchinjwa. Mmemhukumu na kum wua mwenye haki; yeye hakuwapinga.

Subira Na Mateso

Kwa hiyo, ndugu zangu, muwe na subira mpaka Bwana atakapo kuja. Angalieni jinsi mkulima anavyongojea ardhi itoe mavuno mazuri, jinsi anavyongojea kwa subira mvua za mwanzo na za mwisho. Hali kadhalika nanyi muwe na subira. Muwe na mioyo tha biti kwa sababu kuja kwa Bwana kumekaribia. Ndugu zangu, msi nung’unikiane wenyewe kwa wenyewe, ama sivyo mtahukumiwa. Hakimu amesimama mlangoni.

10 Ndugu zangu, kama mfano wa subira wakati wa mateso, waan galieni manabii walionena katika jina la Bwana. 11 Kama mnavy ojua tunawahesabu kuwa wamebarikiwa wale ambao wamevumilia. Mmek wisha kusikia habari za ustahimilivu wa Ayubu na mmeona shabaha ya Bwana, jinsi Bwana alivyo na huruma na rehema.

12 Zaidi ya yote, ndugu zangu, msiape, ama kwa mbingu, au kwa dunia au kwa kiapo kingine cho chote. Bali mkisema ‘Ndio’ iwe ndio, na mkisema ‘Hapana

Maombi Ya Imani

13 Je, kuna mtu ye yote miongoni mwenu aliye na shida? Basi na aombe. Je, yuko mwenye furaha? Basi na aimbe nyimbo za sifa. 14 Je, kuna mtu miongoni mwenu aliye mgonjwa? Basi awaite wazee wa kanisa wamwombee na kumpaka mafuta katika jina la Bwana. 15 Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa huyo na Bwana atamwinua. Kama ametenda dhambi, atasamehewa. 16 Kwa hiyo ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi na kuombeana ili mpate kuponywa. Maombi ya mtu mwenye haki yana nguvu na huleta matokeo.

17 Eliya alikuwa binadamu kama sisi. Aliomba kwa moyo kwamba mvua isinyeshe na mvua haikunyesha juu ya nchi kwa muda wa miaka mitatu na nusu. 18 Kisha akaomba tena na mbingu zikatoa mvua na ardhi ikazaa matunda yake.

19 Ndugu zangu, ikiwa mtu miongoni mwenu anapotoka kutoka katika kweli na mtu mwingine akamrejesha,

Onyo kwa Matajiri na Wachoyo

Sikilizeni, ninyi matajiri! Ombolezeni na kulia kwa sauti kwa ajili ya dhiki inayowajia. Utajiri wenu umeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo. Dhahabu zenu na fedha vimeliwa na kutu! Hiyo kutu itakuwa ni ushuhuda dhidi yenu, na itaila miili yenu kama kwa moto. Mmejilimbikizia mali kwa ajili yenu katika kizazi hiki cha siku za mwisho! Angalieni! Mmeyazuia malipo ya wafanyakazi waliopalilia mashamba yenu. Sasa wananililia! Na kilio cha hao wanaovuna pia kimeyafikia masikio ya Bwana Aliye na Nguvu.

Mmeishi maisha ya anasa duniani na kujifurahisha na kila kitu mlichotaka. Mmeinenepesha miili yenu, kama wanyama walio tayari kwa siku ya kuchinjwa. Mmehukumu na kuua wale watu wasio na hatia, na ambao hawakupingana nanyi.

Uwe Mstahimilivu

Hivyo kina kaka na kina dada, muwe na subira; hadi kuja kwa mara ya pili kwa Bwana. Kumbukeni kuwa mkulima huyasubiria mazao yake yenye thamani yakue ardhini. Huyangoja kwa subira mpaka yapate mvua za masika na za vuli.[a] Hata ninyi pia mnapaswa kungoja kwa subira. Muwe imara mioyoni mwenu, kwa sababu kuja kwa Bwana mara ya pili kumekaribia. Kaka na dada zangu, msiendelee kunung'unikiana ninyi kwa ninyi, ili msije kuhukumiwa kuwa na hatia. Tazameni! Hakimu anasimama mlangoni akiwa tayari kuingia ndani.

10 Kina kaka na kina dada, fuateni mfano wa manabii waliosema kwa jina la Bwana. Wao walipata mateso mengi mabaya lakini walivumilia. 11 Na tunatoa heshima kubwa sana kwa wale wote waliostahimili mateso. Mmesikia juu ya uvumilivu wa Ayubu,[b] na mnayajua ya kuwa baada ya yote hayo Bwana alimsaidia. Hii basi inaonesha ya kuwa Bwana ni mwenye wingi wa rehema na huruma.

Uwe Makini na Unayosema

12 Juu ya mambo yote kaka zangu na dada zangu, usitumie kiapo unapotoa ahadi, Usiape kwa mbingu wala kwa dunia, ama kwa kitu kingine chochote. “Ndiyo” yenu na iwe “Ndiyo halisi”, na “Hapana” yenu na iwe “Hapana halisi”, ili msije mkaingia katika hukumu ya Mungu.

Nguvu ya Maombi

13 Je, miongoni mwenu kuna aliye na shida? Anapaswa kuomba. Je, yupo yeyote mwenye furaha? Anapaswa kuimba nyimbo za sifa. 14 Je, kuna yeyote kwenu aliye mgonjwa? Anapaswa kuwaita wazee wa kanisa kumwombea na kumpaka mafuta katika jina la Bwana. 15 Maombi yanayofanywa kwa imani yatamfanya mgonjwa apone, na Bwana atampa uzima. Kama atakuwa ametenda dhambi, Bwana atamsamehe.

16 Hivyo muungame dhambi ninyi kwa ninyi, na kuombeana ninyi kwa ninyi ili muweze kuponywa. Maombi yanayofanywa na mtu mwenye haki yana nguvu sana na yana matokeo makubwa sana. 17 Eliya alikuwa mwanadamu kama sisi tulivyo. Aliomba kwamba mvua isinyeshe, na haikunyesha katika ardhi kwa miaka mitatu na nusu. 18 Kisha akaomba tena inyeshe, na anga ikatoa mvua, na ardhi ikatoa mazao.

Kuwasaidia Watu Wanapotenda Dhambi

19 Kaka na dada zangu Ndugu zangu, kama mmoja wenu atapotoka katika kweli, na mwingine akamrejeza, 20 yule aliyemrejeza atambue kuwa yule anayemrejeza mtenda dhambi kutoka katika njia yake mbaya ataiokoa roho ya huyo mtu kutoka katika kifo cha milele na atasababisha dhambi nyingi zisamehewe.

Footnotes

  1. 5:7 mvua za masika na za vuli “Mvua za masika” zilinyesha mwanzoni na “mvua za vuli” zilinyesha mwishoni.
  2. 5:11 uvumilivu wa Ayubu Tazama Kitabu cha Ayubu katika Agano la Kale.

Warning to Rich Oppressors

Now listen,(A) you rich people,(B) weep and wail(C) because of the misery that is coming on you. Your wealth has rotted, and moths have eaten your clothes.(D) Your gold and silver are corroded. Their corrosion will testify against you and eat your flesh like fire. You have hoarded wealth in the last days.(E) Look! The wages you failed to pay the workers(F) who mowed your fields are crying out against you. The cries(G) of the harvesters have reached the ears of the Lord Almighty.(H) You have lived on earth in luxury and self-indulgence. You have fattened yourselves(I) in the day of slaughter.[a](J) You have condemned and murdered(K) the innocent one,(L) who was not opposing you.

Patience in Suffering

Be patient, then, brothers and sisters, until the Lord’s coming.(M) See how the farmer waits for the land to yield its valuable crop, patiently waiting(N) for the autumn and spring rains.(O) You too, be patient and stand firm, because the Lord’s coming(P) is near.(Q) Don’t grumble against one another, brothers and sisters,(R) or you will be judged. The Judge(S) is standing at the door!(T)

10 Brothers and sisters, as an example of patience in the face of suffering, take the prophets(U) who spoke in the name of the Lord. 11 As you know, we count as blessed(V) those who have persevered. You have heard of Job’s perseverance(W) and have seen what the Lord finally brought about.(X) The Lord is full of compassion and mercy.(Y)

12 Above all, my brothers and sisters, do not swear—not by heaven or by earth or by anything else. All you need to say is a simple “Yes” or “No.” Otherwise you will be condemned.(Z)

The Prayer of Faith

13 Is anyone among you in trouble? Let them pray.(AA) Is anyone happy? Let them sing songs of praise.(AB) 14 Is anyone among you sick? Let them call the elders(AC) of the church to pray over them and anoint them with oil(AD) in the name of the Lord. 15 And the prayer offered in faith(AE) will make the sick person well; the Lord will raise them up. If they have sinned, they will be forgiven. 16 Therefore confess your sins(AF) to each other and pray for each other so that you may be healed.(AG) The prayer of a righteous person is powerful and effective.(AH)

17 Elijah was a human being, even as we are.(AI) He prayed earnestly that it would not rain, and it did not rain on the land for three and a half years.(AJ) 18 Again he prayed, and the heavens gave rain, and the earth produced its crops.(AK)

19 My brothers and sisters, if one of you should wander from the truth(AL) and someone should bring that person back,(AM) 20 remember this: Whoever turns a sinner from the error of their way will save(AN) them from death and cover over a multitude of sins.(AO)

Footnotes

  1. James 5:5 Or yourselves as in a day of feasting