Yesu Amponya Mtu Penye Bwawa La Bethzatha

Baada ya haya, Yesu alikwenda tena Yerusalemu kuhudhuria sikukuu mojawapo ya Wayahudi. Huko Yerusalemu, karibu na mlango uitwao Mlango wa Kondoo, pana bwawa moja ambalo kwa Kiebrania linaitwa Bethzatha ambalo lina baraza tano zenye safu za matao. Wagonjwa wengi sana, vipofu, viwete, na waliopooza walingojea kwenye baraza hizo. Walikuwa wakisubiri maji yatibuliwe, [ kwa maana malaika wa Bwana alikuja mara kwa mara akayatibua maji na yule aliyekuwa wa kwanza kuingia bwawani baada ya maji kutibuliwa alipona ugonjwa wo wote aliokuwa nao.]

Mmoja wa wagonjwa waliokuwepo alikuwa ameugua kwa muda wa miaka thelathini na minane. Yesu alipomwona amelala hapo, na akijua kwamba amekuwa katika hali hiyo kwa muda mrefu, alimwul iza, “Unataka kupona?” Yule mgonjwa akajibu, “Bwana, sina mtu wa kuniingiza bwawani maji yanapotibuliwa. Ninapoanza kwenda bwawani, mgonjwa mwingine huniwahi akaingia kabla yangu.” Yesu akamwambia, “Simama, chukua mkeka wako, utembee!” Mara moja yule mtu akapona, akachukua mkeka wake, akaanza kutembea! Jambo hili lilitokea siku ya sabato. 10 Kwa hiyo Wayahudi wakamwambia yule mtu aliyeponywa, “Leo ni sabato. Huruhusiwi kubeba mkeka wako.”

11 Yeye akawajibu, “Yule mtu aliyeniponya aliniambia, ‘Chu kua mkeka wako utembee.”’

12 Wakamwuliza, “Ni mtu gani huyo aliyekuambia uchukue mkeka wako utembee?”

13 Yule mtu aliyeponywa hakufahamu ni nani aliyemponya kwa sababu palikuwa na umati mkubwa wa watu na Yesu alikuwa amepe nyezea humo akaondoka.

14 Baadaye Yesu alimkuta yule aliyemponya Hekaluni akamwam bia, “Sasa umepona. Angalia usitende dhambi tena usijepatwa na jambo baya zaidi.”

15 Yule mtu akaenda, akawaambia wale Wayahudi kuwa ni Yesu aliyemponya.

16 Kwa sababu Yesu alikuwa amemponya siku ya sabato, wal ianza kumsumbua. 17 Yesu akawaambia, “Baba yangu anafanya mema siku zote. Mimi pia sina budi kufanya mema.” 18 Maneno haya yaliwaudhi sana viongozi wa Wayahudi. Wakajaribu kila njia wapate kumwua, kwa sababu, zaidi ya kuvunja sheria za sabato, alikuwa akijifanya sawa na Mungu kwa kujiita Mwana wa Mungu.

Mamlaka Ya Mwana

19 Yesu akawajibu, “Ninawaambia hakika, Mwana hawezi kufa nya jambo lo lote mwenyewe isipokuwa lile alilomwona Baba yake akifanya; na lo lote alifanyalo Baba, Mwana pia hulifanya. 20 Kwa kuwa Baba anampenda Mwana na anamwonyesha mambo yote afa nyayo; pia atamwonyesha hata mambo makubwa kuliko haya, ambayo yatawastaajabisha. 21 Kama vile Baba awafufuavyo wafu na kuwapa uzima, vivyo hivyo Mwana huwapa uzima wale awapendao. 22 Baba hamhukumu mtu ye yote, mamlaka ya kuhukumu amemwachia Mwana; 23 ili kila mtu amheshimu Mwana kama amheshimuvyo Baba. Ye yote anayekataa kumheshimu Mwana, anakataa kumheshimu Baba aliyemtuma. 24 Ninawaambia hakika, ye yote anayesikiliza maneno yangu na kumwamini yule aliyenituma, anao uzima wa milele na hatahukumiwa. Amevuka kutoka kwenye mauti, na kuingia katika uzima. 25 Nina waambia hakika, wakati utafika, tena umekwisha timia, ambapo wafu wataisikia sauti ya Mwana wa Mungu; na wote watakaoisikia wata kuwa hai. 26 Kama vile Baba alivyo chanzo cha uzima, hali kad halika amemwezesha Mwanae kuwa chanzo cha uzima. 27 Na amempa Mwanae mamlaka ya kuhukumu kwa kuwa yeye ni Mwana wa Adamu.

28 “Msishangae kusikia haya. Wakati unakuja ambapo wafu wataisikia sauti yake, 29 nao watatoka makaburini; wale waliot enda mema watafufuka na kuwa hai, na wale waliotenda maovu, wata fufuka na kuhukumiwa. 30 Mimi siwezi kufanya jambo lo lote kwa mamlaka yangu mwenyewe. Mimi nahukumu kufuatana na jinsi Mungu anavyoniambia. Na hukumu yangu ni ya haki kwa kuwa sitafuti kufa nya nipendavyo, bali nafanya mapenzi yake yeye aliyenipeleka.”

Mashahidi Wa Yesu

31 “Kama ningekuwa najishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu usingekuwa na uzito. 32 Lakini yupo mwingine anishuhudiaye na ninafahamu kwamba ushuhuda wake ni wa kweli. 33 Mliwapeleka wajumbe wenu kwa Yohana, naye akashuhudia iliyo kweli. 34 Si kwamba ninategemea ushuhuda wa mwanadamu, la, bali ninalitaja hili kusudi ninyi mpate kuokolewa. 35 Yohana alikuwa taa iliy owaka na kuwaangazia, na kwa muda mlikubali kufurahia nuru yake.

36 “Lakini ninao ushuhuda mzito zaidi kuliko wa Yohana. Kazi ambayo Baba amenituma nikamilishe, naam , ishara hizi nina zofanya, zinashuhudia kuwa Baba ndiye aliyenituma. 37 Na Baba aliyenituma naye amenishuhudia. Hamjapata kamwe kuisikia sauti yake wala kuiona sura yake. 38 Wala ujumbe wake hamuupokei maana hamumwamini aliyemtuma.

39 “Mnasoma Maandiko kwa bidii kwa maana mnafikiri kuwa humo mtapata uzima wa milele. Maandiko hayo hayo ndio yanayonish uhudia mimi. 40 Lakini mnakataa kuja kwangu kupata uzima.

41 “Mimi sitafuti kutukuzwa na watu. 42 Lakini, ninajua kwamba hamna upendo wa Mungu mioyoni mwenu. 43 Mimi nimekuja kwa jina la Baba yangu na mnakataa kunipokea. Lakini mtu mwingine akija kwa jina lake mwenyewe, mtampokea. 44 Ndio maana hamwezi kuamini! Mnapenda sana kusifiana wenyewe kwa wenyewe wala ham jishughulishi kutafuta sifa kutoka kwake ambaye peke yake ndiye

Mungu!

45 “Msidhani kuwa mimi nitawashtaki kwa Baba. Anayewashtaki ni huyo Musa ambaye mnamwekea matumaini yenu. 46 Kama kweli mli kuwa mmemwamini Musa, mngaliniamini na mimi kwa maana aliandika kunihusu mimi. 47 Lakini ikiwa hamwamini aliyoandika Musa, mtaaminije ninayoyasema?”

Yesu Amponya Mtu Bwawani

Baadaye, Yesu akaenda Yerusalemu kwa ajili ya sikukuu maalumu ya Wayahudi. Huko Yerusalemu kulikuwa na bwawa lenye mabaraza matano. Kwa Kiaramu liliitwa Bethzatha.[a] Bwawa hili lilikuwa karibu na Lango la Kondoo. Wagonjwa wengi walikuwa wamelala katika mabaraza pembeni mwa bwawa. Baadhi yao walikuwa wasiyeona, wengine walemavu wa viungo, na wengine waliopooza mwili.[b] Nyakati zingine malaika wa Bwana alishuka bwawani na kuyatibua maji. Baada ya hapo, mtu wa kwanza aliyeingia bwawani aliponywa ugonjwa aliokuwa nao.[c] Mmoja wa watu waliolala hapo alikuwa mgonjwa kwa muda wa miaka thelathini na minane. Yesu alimwona akiwa amelala hapo na kutambua kuwa amekuwa mgonjwa kwa muda mrefu sana. Hivyo akamwuliza, “Je, unataka kuwa mzima?”

Yule mgonjwa akajibu, “Bwana, hakuna mtu wa kunisaidia kuingia kwenye bwawa mara maji yanapotibuliwa. Najitahidi kuwa wa kwanza kuingia majini. Lakini ninapojaribu, mtu mwingine huniwahi na kuingia majini kabla yangu.”

Kisha Yesu akasema, “Simama juu! Beba kirago chako na utembee.” Mara hiyo, mtu huyo akapona. Akabeba kirago chake na kuanza kutembea.

Siku yalipotokea haya yote ilikuwa ni Siku ya Sabato.[d] 10 Hivyo baadhi ya Wayahudi wakamwambia yule mtu aliyeponywa, “Leo ni Sabato. Kulingana na sheria yetu wewe hauruhusiwi kubeba mkeka katika siku ya Sabato!”

11 Lakini yeye akajibu, “Yule mtu aliyeniponya aliniambia, ‘Beba mkeka wako uende.’”

12 Wakamwuliza, “Ni nani aliyekuambia kubeba mkeka wako na kutembea?”

13 Lakini yule mtu aliyeponywa hakuwa amemfahamu ni nani. Walikuwepo watu wengi hapo, na Yesu alikwisha kuondoka.

14 Baadaye, Yesu akamwona huyo mtu Hekaluni na akamwambia, “Tazama, umepona sasa. Kwa hivyo uache kutenda dhambi tena, la sivyo jambo baya zaidi laweza kukupata.” 15 Kisha huyo mtu akaondoka na kurudi kwa wale Wayahudi waliomuuliza. Naye aliwaeleza kuwa Yesu ndiye aliyemponya.

16 Yesu alikuwa anayafanya yote haya katika siku ya Sabato. Hivyo Wayahudi hao wakaanza kumsumbua asiendelee. 17 Lakini yeye akawaambia, “Baba yangu hajawahi kuacha kufanya kazi, hivyo nami pia nafanya kazi.” 18 Hili likawafanya waongeze juhudi ya kumwua. Wakasema, “Mwanzoni mtu huyu alikuwa anavunja sheria kuhusu siku ya Sabato. Kisha akasema kwamba Mungu ni Baba yake! Yeye anajifanya kuwa yuko sawa na Mungu.”

Yesu Anayo Mamlaka ya Mungu

19 Lakini Yesu akajibu, “Hakika nawaambieni kuwa Mwana hawezi kufanya chochote peke yake. Bali hufanya tu yale anayoona Baba yake anayafanya. Kwa maana Mwana hufanya mambo ambayo Baba huyafanya. 20 Baba anampenda Mwana na humwonesha kila kitu anachofanya. Pia Baba atamwonesha Mwana mambo makuu ya kufanya kuliko hili. Kisha nyote mtashangazwa. 21 Baba huwafufua wafu na kuwapa uzima. Kwa njia hiyo hiyo, Mwana pia huwapa uzima wale anaowataka.”

22 “Vile vile, Baba hamhukumu mtu. Bali amempa Mwana nguvu ya kufanya hukumu zote. 23 Mungu alifanya hivi ili watu wote waweze kumheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Mtu yeyote asiyemheshimu Mwana hamheshimu Baba. Kwani Baba ndiye aliyemtuma Mwana.

24 Kwa hakika nawaambia, yeyote anayesikia ninayosema na kumwamini yule aliyenituma anao uzima wa milele. Hawa hawatahukumiwa kuwa na hatia. Kwani tayari wameshaivuka mauti na kuingia ndani ya uzima. 25 Mniamini, wakati muhimu sana unakuja. Wakati huo tayari upo ambapo watu waliokufa wataisikia sauti ya Mwana wa Mungu. Na hao watakaoisikia watafufuka na kuwa hai. 26 Uzima huja kutoka kwa Baba mwenyewe. Na pia Baba amemruhusu Mwana kutoa uzima. 27 Na Baba amempa Mwana mamlaka ya kuwahukumu watu wote kwa sababu yeye ndiye Mwana wa Adamu.

28 Ninyi msishangazwe na hili. Wakati unakuja ambapo watu wote waliokufa na kuwamo makaburini mwao wataisikia sauti yake. 29 Kisha watatoka nje ya makaburi yao. Wale waliotenda mema watafufuka na kupata uzima wa milele. Lakini wale waliotenda maovu watafufuka na kuhukumiwa kwa kuwa na hatia.

30 Siwezi kufanya jambo lolote peke yangu. Ninahukumu kama vile ninavyoagizwa. Na hukumu yangu ni halali, kwa sababu sitafuti kujifurahisha mwenyewe. Bali ninataka tu kumfurahisha yeye aliyenituma.”

Yesu Asema Zaidi Na Viongozi wa Kiyahudi

31 “Endapo nitawaeleza watu mambo yangu mwenyewe, watu hawatakuwa na uhakika kama yale ninayosema ni kweli. 32 Lakini yupo mwingine anayewaeleza watu mambo yangu, nami nafahamu kuwa yale anayoyasema juu yangu ni kweli.

33 Mliwatuma watu kwa Yohana, naye akawaambia yaliyo kweli. 34 Hivyo sihitaji mtu yeyote wa kuwaeleza watu juu yangu, isipokuwa nawakumbusha ninyi yale aliyoyasema Yohana ili muweze kuokolewa. 35 Yohana alikuwa kama taa iliyowaka na kutoa mwanga, nanyi mlipata raha mkiufurahia mwanga wake japo kwa muda.

36 Hata hivyo uthibitisho nilionao mwenyewe juu yangu ni mkuu kuliko chochote alichokisema Yohana. Mambo ninayofanya ndiyo yanayonithibitisha. Haya ndiyo Baba aliyonipa kufanya. Nayo yanadhihirisha kuwa Baba alinituma. 37 Na Baba aliyenituma yeye mwenyewe ametoa uthibitisho juu yangu. Lakini hamjawahi kabisa kuisikia sauti yake. Hamjawahi pia kuuona uso wake jinsi ulivyo. 38 Mafundisho ya Baba hayakai ndani yenu, kwa sababu hamumwamini yule aliyetumwa na Baba. 39 Mnajifunza Maandiko kwa makini. Nanyi mnafikiri kuwa yanawapa uzima wa milele. Maandiko haya haya yanaeleza habari zangu! 40 Lakini mnakataa kuja kwangu kuupata huo uzima.

41 Sitaki kutukuzwa nanyi ama na mwanadamu mwingine yeyote. 42 Hata hivyo ninawajua ninyi, na ninajua kwamba hamna upendo kwa Mungu. 43 Nimekuja kutoka kwa Baba yangu nami ni msemaji wake, lakini hamnikubali. Lakini watu wengine wakija wakijisemea mambo yao tu, mnawakubali! 44 Ninyi mnapenda kupeana sifa kila mmoja kwa mwenzake. Lakini hamjaribu kupata sifa zinazotoka kwa Mungu wa pekee. Hivyo mtawezaje kuamini? 45 Msifikiri kwamba mimi ndiye nitakayesimama mbele za Baba na kuwashtaki. Musa ndiye atakayewashtaki. Na ndiye mliyetegemea angeliwaokoa. 46 Kama kwa hakika mlimwamini Musa, nami mlipaswa kuniamini, kwa sababu yeye aliandika habari juu yangu. 47 Lakini hamuyaamini aliyoyaandika, hivyo hamuwezi kuyaamini ninayoyasema.”

Footnotes

  1. 5:2 Bethzatha Pia huitwa Bethsaida au Bethesda. Ama bwawa la maji lililoko kaskazini mwa Hekalu kule.
  2. 5:3 Nakala zingine za Kiyunani zimeongeza, “na husubiri maji yatibuliwe”.
  3. 5:4 Nakala zingine za baadaye ziliongeza mstari wa 4, hivyo kutenganisha mstari wa 4 na wa 5: “Nyakati zingine malaika wa Bwana alishuka bwawani na kuyatibua maji. Baada ya hapo, mtu wa kwanza aliyeingia bwawani aliponywa ugonjwa aliokuwa nao.”
  4. 5:9 Siku ya Sabato Ilikuwa siku maalumu kwa Waisraeli na Wayahudi. Kwa amri ya Mungu siku hiyo ilitengwa kama siku ya mapumziko na ya kumheshimu Mungu.